ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, March 22, 2012

MUAMBA ALIFARIKI KWA DAKIKA 78

Fabrice Muamba ''alifariki'' kwa dakika 78 baada ya kuzirai uwanjani, amebainisha daktari wa klabu yake ya Bolton Wanderers' Jonathan Tobin.

Lakini Dr Tobin amesema ameshangazwa na jinsi mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 23 alivyoweza kuponyoka hadi wakati huu.

Katika mahojiano yenye makiwa, Dr.Tobin amesema hatukua na hakika, fikra zetu ziliwaza mengine kabisa hatukutazamia kufikia hali hii ya afuweni kiasi hiki. Ni ajabu. Muamba alizirai kutokana na kukwama kwa mishipa ya moyo wakati wa mchuano wa Kombe la FA kwenye uwanja wa White Hart Lane jumamosi iliyopita.

Alisema kua Muamba alipewa vifaa viwili vya kumsaidia kuikunjua mishipa ya moyo mara ya kwanza uwanjani mara ya pili wakati akipitishwa uwanjani na mara nyingine 13 kwenye gari la wagonjwa kuelekea hospitali lakini ajabu ni kwamba hakuna hata moja lililofanikiwa.

Saa mbili baada ya leo kurejesha fahamu, nilimsogelea na kumuuliza jina lake, akajibu,Fabrice Muamba. Nikasema nasikia wewe ni mchezaji mzuri wa mpira' akasema'Najitahidi' Nilijihisi chozi likinitoka.'' Mtaalamu ameongezea kusema kua: "singependa kuahidi muujiza kwa wakati huu lakini kwa hali ilivyo maisha yake hayamo hatarini tena.

Bado ni mapema mno kusema kwa uhakika kama atarudi kucheza mpira au la. Dr Sam Mohiddin, mshauri wa masauala ya magonjwa ya Moyo anayemuangalia Muamba kwa sasa, alisema kua Fabrice amezidi kuonyesha dalili nzuri za kupona.

Matokeo yake yamekua ya ajabu kutokana na utunzaji usio wa kawaida. Hali ya afya yake imetushangaza sana. "Jambo la muhimu ni jinsi alivyotunzwa mara tu alipoanguka na kuzirai uwanjani, huduma ya haraka na hasa majaribio ya kuamsha moyo wake uwanjani White Hart Lane na wakati wa kusafirishwa kuelekea hospitali.

Kwa sasa kurejelea maisha yake ya kawaida ni jambo lenye uwezekano mkubwa.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.