ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, March 9, 2012

LIGI TAIFA NGAZI YA MKOA WA MWANZA YAANZA

Misungwi Stars.

Nange Fc.

Jukwaa kuu uwanja wa Mwanakanenge wilayani Misungwi.

Sehemu ya Mashabiki mchezoni.

Ligi ya Taifa ngazi ya mkoa wa Mwanza imeanza leo katika uwanja wa Mwanakanenge wilayani misungwi kwa mchezo kati ya Misungwi Stars na Nange Fc matokeo Misungwi stars wametoka kifua mbele kwa ushindi wa 4-1.

Iliwachukuwa dakika mbili tu timu ya Misungwi Stars kujipatia bao la kwanza kupitia mshambuliaji wake Godwin Mganga, dakika ya 10 goli la pili, la tatu dakika 35 kupitia Kulwa Mahamoud na Selemani kisendi alishindilia msumari wa mwisho dakika ya 89. Goli la kufutia machozi kwa Nange Fc lilipatikana dakika ya 13 kipindi cha kwanza.

Ligi hiyo itaendelea tena kesho mchezo kati ya Nyamagana United watakaoshuka dimbani dhidi ya Chanel Afrika.

Nako kituo cha Geita uwanja wa Katolo mchezo utachezwa kati ya West Boyz na Polisi Geita.

Ligi ya kusaka nane bora ngazi ya mkoa inashirikisha timu 19 zilizojigawa katika makundi manne.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.