ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Monday, February 6, 2012

MKOMBOZI BANK YAZINDUA TAWI MWANZA

Utepe ukikatwa kama ishara ya uzinduzi wa tawi la pili la Benki ya Mkombozi, ulizinduliwa rasmi leo asubuhi na Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Catholic la Mwanza, Thadues Ruwaaiich.

Mkurugenzi Mtendaji wa Benki hiyo, Edwina Lupembe amesema kuwa tawi hilo la benki lililofunguliwa jijini Mwanza ambalo ni la pili nchini, limeanzishwa kwa lengo la kutoa huduma za kibenki sanjari na kushughulika na matatizo ya kiuchumi kwa jamii katika nyanja mbalimbali.

Mr M. A Kashonda moja kati ya Board Member
“Hasa benki yetu imewalenga watu wenye kipato cha chini kwa kutoa huduma hizo zikiwemo za akiba, mikopo na kutuma fedha na walengwa wakuu ni wananchi wote na hasa wale wenye vipato vya chini ikiwa ni pamoja na kuwaendeleza katika kilimo kwanza”,

Katika kipindi cha miaka miwili na nusu tangu benki hiyo ianzishwe tangu ilipofungua milango yake hadi Desemba 31mwaka huu, raslimali za benki hiyo zimekua hadi kutoka shilingi bilioni 7 Septemba 2009 hadi kufikia shilingi bilioni 33.49.

Sehemu ya mahudhurio ya ufunguzi huo uliofanyika barabara ya Nyerere jijini Mwanza.

Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Catholic la Mwanza, Thadues Ruwaaiich akifungua akaunti katika benki hiyo.

Mazungumzo ya hapa na pale na mkurugenzi.

Askofu Paul Lunzoka kutoka Tabora ambaye aliungana na wana Mwanza kwaajili ya tukio la uzinduzi naye akifungua akaunti katika benki hiyo.

Ni mafanikio makubwa kwani ni siku ya kwanza tu lakini wengi wamejitokeza kufungua akaunti katika benki hii.

Mdau wa Mkombozi benki akitoa maelezo kwa wateja.

Baadhi ya wafanyakazi Mkombozi Bank wakipata flash.

Picha ya pamoja na mama Mkurugenzi.

Baba Askofu pamoja na Board Members.

Baba Askofu pamoja na Wafanyakazi.

Benki hii imeanzishwa kama ilivyo kwa huduma nyingine zinazotolewa na Kanisa Katoliki kama vile shule na hospitali huku walengwa wakuu wakiwa ni wananchi wenye kipato cha chini pamoja na kuendeleza kilimo.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.