ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, February 8, 2012

MGOMO BUGANDO SASA NI LIVE MEMO ZABANDIKWA UONGOZI WAMTUPIA MKUU WA MKOA KUTOA KAULI

Baba wa Edina Julis (10) akiwa amembeba mtoto wake mwenye maumivu makali ya mguu wakirundi nyumbani baada ya kukosa huduma leo katika hospitali ya Bugando...hata hivyo baadhi ya wauguzi wa kliniki ya mifupa wamemshauri baba huyo kumpeleka mtoto wake katika hospitali binafsi baada ya kuhisi huenda tatizo la mtoto huyo kuwa kubwa kama atakaa bila yaa kupata huduma.

Yaliyojiri leo Hospitali ya rufaa Bugando jijini Mwanza mgomo upo tena unafukuta chini kwa chini na memo tayari zimebandikwa kwenye baadhi ya milango ya vyumba vya mikutano ya wanataaluma wa utibabu tangu jana, Uongozi unakigugumizi kulizungumzia hili na kuweka bayana.

Tangazo linasema:-Kuanzia leo tarehe 7/2/2012 siku ya jumanne saa sita mchana tunataarifu kuwa tunasitisha huduma zote zikiwemo zile za dharula hadi hapo serikali itakapotimiza madai yote yanayosimamiwa na kamati kuu ya madaktari Tanzania. Imetolewa na jumuiya ya Madaktari bugando (Residents, Registrers,Interns)

Huku akipinga kauli iliyoripotiwa na baadhi ya Vyombo vya habari kuhusu yeye kuagiza wagonjwa kuja toka mikoa mbalimbali nchini kuja kupata huduma hospitalini hapa, Kaimu mkurugenzi wa Hospitali ya Bugando Dr.Japhet Giliyoma hakuwa tayari kuelezea bayana hali halisi akisisitiza kuwa mkuu wa mkoa ndiye atakayetoa taarifa rasmi kwani tayari wamekwisha mpatia hali halisi.

Mapokezi wagonjwa wengi wamelalamikia suala la kupigwa tarehe kurejea wiki kadhaa zijazo...

"Naitwa Rehema Wasongwa tareha 25 nilikuja wakanipa tarehe ya leo, leo nimekuja wamenipiga tarehe wiki mbili kurudi tena mimi masikini nitafanyaje na ninasafiri kutoka Musoma hadi Mwanza kuitafuta huduma?"

Julius Lutabi baba wa mtoto Edna aliyegongwa na gari toka jumamosi iliyopita, yuko hapa tangu asubuhi jibu limetoka akipigwa tarehe mpaka.... ameiomba serikali kusitisha mijadala mingine na kuigeukia wizara ya afya.

Mwendo ni kupigwa karenda tuu wengi wamekosa huduma...

Jamani hata kitengo cha ULTRASOUND kama zipo vile...

Shughuli nyingine zinaendelea kama kawa lakini matibabu mmmh!...

Wadau wa habari na sehemu ya wafanyakazi wa hospitali wakipata taarifa toka kwa kaimu mkurugenzi.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.