ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, January 26, 2012

UHAMISHO ASKALI KITENGO CHA KUDHIBITI DAWA ZA KULEVYA MWANZA WAFANYWA KUWANUFAISHA WAHUJUMU?...?

Baadhi ya wakazi wa mkoa wa Mwanza wamelalamikia uhamisho wa askali mpelelezi kitengo cha kudhibiti dawa za kulevya jijini hapa, Benson Kalokola na kumuomba mkuu wa jeshi la Pilisi nchini (IGP) Said Mwema kubatilisha uhamisho huo vinginevyo wataandamana.Afande Kalokola (L) akitunukiwa zawadi ya utumishi bora na mkuu wa mkoa wa Mwanza Erenest Ndikilo katika hafla iliyofanyika hivi karibuni ndani ya ukumbi wa ofisi za jeshi la polisi mkoa wa Mwanza kwa chati Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza Liberatus Barlow katikati akishuhudia tukio hilo.
Askali huyo amefanikiwa kwa kiwango kikubwa kudhibiti uingizwaji na uuzwaji holela wa dawa hizo jijini hapa na kwamba kitendo cha kumhamisha kimelenga kuruhusu biashara hiyo haramu kushamiri.

Kalokola ambaye hivi karibuni akiwa na askali wenzake tisa, aliongoza mapambano ya kujibizana kwa risasi na majambazi matano kisha kuyaua wakati yalipotaka kupora katikati ya jiji.Kikosi kazi cha kupambana na madawa ya kulevya toka jeshi la polisi mkoa wa Mwanza na nishani zao.

Kama hiyo haitoshi Afande Kalokola ndiye aliyefanikisha zoezi la kutokomeza mauaji ya walinzi waliokuwa wakiuawa kila kukicha miezi kadhaa iliyopita katika mitaa ya jiji la Mwanza na kukatwakatwa kwa mapanga vipande vipande, hatimaye kumnasa mganga wa jadi aliyekuwa akiagiza damu za walinzi hao kwaajili ya kufanya zindiko kwa sehemu za wavuvi na machimbo ya madini.

Uhamisho huo wa kumtoa mpiganaji' huyo jijini Mwanza na kumpeleka mkoani Manyara unatajwa na wengi wachambuzi wa mambo kuwa ni zengwe na shinikizo kutoka kwa matajiri wanaojihusisha na biashara mbalimbali haramu anaowaumbua au pengine kukamata mizigo yao haramu.


CHA AJABU; mara baada ya taarifa za uhamisho kusikika baadhi ya askali wa beria za kukagua mizigo inayoingia na kutoka jijini Mwanza wameonekana kupiga shangwe juu ya uhamisho huo.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.