ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Tuesday, January 3, 2012

HOT NYUZI ZA MAGAZETI YA LEO

KAULI ya Waziri wa Ujenzi, Dk John Magufuli kwamba watakaoshindwa kulipa nauli mpya ya Sh200 kuvuka Kigamboni ni vyema wakapiga mbizi kuvuka bahari, imewakera wabunge wa Mkoa wa Dar es Salaam ambao sasa wanamtaka aombe radhi.

Juzi, Dk Magufuli akiwa katika ziara eneo la Kivukoni alijaribu kuzungumza na wananchi wa Kigamboni kuhusu ongezeko hilo la nauli lakini badala ya wananchi hao kumsikiliza, walizomea ndipo alipowaambia kuwa watakaoshindwa ni vyema wakapiga mbizi baharini, kuzunguka Kongowe kuingia katikati ya jiji au warudi kijijini wakalime.jana, wabunge hao licha ya kumtaka Dk Magufuli aombe radhi, wameitaka Serikali kusitisha mara moja amri ya ongezeko hilo la nauli katika kivuko hicho kutokana na uamuzi huo kufikiwa bila ya kuwashirikisha wananchi.....

BAADHI ya madiwani, wenyeviti wa serikali za vijiji kupitia NCCR MAGEUZI katika Jimbo la Kigoma Kusini pamoja na wanachama, wamesema watajiuzulu nyadhifa zao zote za serikali na kurudisha kadi ikiwa mbunge wa jimbo hilo, David Kafulila, atavuliwa uanachama na kupoteza ubunge.

Katika Jimbo la Kigoma Kusini, NCCR-Mageuzi inaongoza vijiji nane na ina madiwani wanne katika kata za Nguruka, Itebula, Mgaza na Kandaga.......

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.