ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Monday, January 16, 2012

KITAANI KWETU MAJI SPESHO HAYANA LADHA.....!

Maji haya yanahifadhiwa kwenye chupa za makampuni tofauti tofauti (dasano, kilimanjari, uhae, akwa roku na etc), chupa zinazokusanywa mara baada ya kutumika kisha zinafungwa vizuri bila 'sildi' nakuwekwa kwenye friji..dakika kadhaa kitu briiidi kinaingia sokoni...
Wakati yale spesheli @ chupa ni shilingi 500/= bei kwa chupa moja kwa maji haya ni shilingi 100/= hadi 200/= tu...!

Wateja wakuu wa maji haya ya kunywa ni madreva wa daladala, makonda, mamantilie na wateja wao magengeni, wachuuzi wa samaki na mbogamboga sokoni, wadau minadani, baadhi ya madreva wa pikipiki, makuli aka wabeba mizigo masokoni, wanafunzi wa shule za msingi na kadhalika....

Utayarishaji wa maji haya: hayachemshwi bali huwekwa water guard kisha yakachujwa, ukiuliza kwanini hayachemshi wadau wanasema kuni mzigo mmoja ni shilingi 1,500 na hazitoshi kuchemsha maji hivyo hutumia njia rahisi isiyo na gharama kuyasafisha kwa water guard.

Ila sasa kuna wengine hata hiyo water guard hawaweki bali huyachuja na kuyauza juu kwa juu...

Katika pitapita yangu nakutana na mjasiliamali huyu, muuza maji ya kunywa wateja wake wanasema maji ya kuchemsha "oooh... hayana ladha..." wengine "oooh... nikinywa maji ya kuchemsha tumbo linauma" MWINGINE akanigusa nikamwelewa Yaani nitoe 500/= kununua maji wakati kipato changu chenyewe kwa siku 500/=?

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.