ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, January 4, 2012

BREAKING NEWS: HAMAD RASHID ATIMULIWA CUF

Hamad Rashid na wenzie wame- timuliwa uanachama kwa chama cha Wananchi CUF, hivyo kiongozi huyo mahiri mwenye ushawishi mkubwa ndani ya chama kukosa sifa za kuendelea kuwa Mbunge wa chama hicho kwa jimbo la Wawi.

Hivi karibuni Mbunge huyo alifika kwenye Kata ya Manzese jijini Dar es salaam ili kufanya mkutano na wanachama lakini ghafla watu wanaodaiwa kutoka makao makuu ya chama hicho, walifika Manzese na kufanya vurugu wakizuia asifanye mkutano.

Wachunguzi wa karibu wa sakata hili na chanzo cha kutemwa kwa Hamad Rashid, wananyetisha kuwa hili limetokea kutokana na kumekuwepo kwa malumbano ya sera na madaraka baina ya Maalim Seif na Hamad ambaye alitangaza hadharani kwamba atawania nafasi ya Katibu Mkuu wa CUF inayoshikiliwa na Maalim Seif.

Nia ya Hamad kuwania nafasi hiyo imeonyesha dhahiri kumtikisa Maalim Seif ambaye kwa siku za hivi karibuni alinukuliwa akijibu kauli hiyo kwa kusema kama ana ubavu asubiri uchaguzi.

Jeh! picha litaendeleaje...?

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.