ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, March 19, 2011

RAIS KIKWETE AMPONGEZA ASKOFU MPYA JIMBO LA KANISA KATOLIKI DODOMA KATIKA WAKFU LEO.

Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akimpongeza askofu mpya wa jimbo Katoliki Dodoma Mwashamu Gervas Johnn Nyaisonga muda mfupi mara baada ya kumaliza ibada ya kumweka wakfu askofu huyo iliyofanyika katika kanisa kuu la mtakatifu Paulo Msalaba mjini Dodoma leo asubuhi.

Mwadhama Polycarp Pengo akimvika kofia ya Kiaskofu Muashamu Gervas John Nyaisonga wakati wa ibada hiyo. Kushoto ni Rais wa baraza la maaskofu kanisa katoliki Tanzania Muashamu Yuda Thadeus Ruwainchi ambaye ambaye amehamishiwa jimbo kuu la Mwanza akiwa tayari amesimikwa.

Mwadhama Polycarp Pengo (katikati) akiongoza ibada ya kumweka wakfu mhashamu Gervas John Nyaisonga (aliyelala chini) kuwa askofu mpya wa Jimbo Katoliki Dodoma.
PICHA ZOTE NA FREDDY MARO.

STONE CLUB aka ZE JIWE LEO PATAMUuuuu!!!..

'HahaaaaaAAAAAaaaa'
Ni time ya kuGONga cHiAZ MarA bAAda ya kUTOKa sAfARi kUPoKeA kikombe cHa bABu
USiuliZE nI wAPi 'STONE CLUB' tHe oNE aND oNLY.

KIMTINDO DOTI COM.

Kuna mvua kinoma leo AR. kwani imenyesha tangu kunakucha hadi mishale ya mchana kati, hapa ni moja ya kitaa Makao mapya.

Uhuru road ni katikati ya jiji la Arusha.

Ubunifu muhimu..

Anaza side yaani ni full mikoba na saundi ya mtikisiko..

Majira ya jioni ndani ya Arachuga ni mtungo jazz kwa kwenda mbele..

FM ACADEMIA WAMWAGA BURUDANI ARUSHA.

Sauti adimu ya Jose Mara 'Imara kama mnara'

Le Presider' Nyoshi el Saadat akifanya mambo usiku jana ndani ya The blue triple A club.

Mule mule FBI.

Le Dance de Ngwasuma.

Ngwasuma from the Top of stage to the dancing flo'.

Friday, March 18, 2011

UJUMBE WANGU WIKIENDI HII : POMBE SIYO CHAI.

Marafiki wamemfanya kitu mbaya men.

Na huyu wakamning'iniza men.

Ayaaa!! Jadili men.

BASI ZUKA LEO LIPS CLUB MWANZA TUONE

Ukiwa Isamilo Lodge Mwanza na ukathubutu kuzama shimo la ladha chumba cha ngoma za raha makulaji na vinywaji utasikia--.. pRAkAtA tUMBa-tUMBa-TuMBA-tUMBa-tUMBa'''''''@@@@@##** !!!!!!!!!!!!!HuU ndO mPaNGo.

NISHATI YA GASS YAJA?

Frederick Katulanda ameandika...
Serikali ilieleza kuwa itashusha bei ya nishati Gass ili wanzania wote wamudu kuitumia na kuepukana na utumiaji wa mkaa kupunguza uharibifu wa mazingira. Je, ahadi hiyo imetekelezwa, na kama ni kweli ni watanzania wangapia wameacha kutumia mkaa na sasa wanatumia Gass?

MAGUFULI AJIUZULU........??.............!

Kuna taarifa zisizothibitishwa kwamba waziri wa ujenzi John Magufuli amejiuzulu wadhifa huo. Taarifa za kuaminika toka serikalini zimepasha kuwa waziri huyo amemuandikia barua Rais Jakaya Kikwete, akimtaarifu uamuzi wake wa kujiuzulu baada ya kufadhaishwa na hatua ya Waziri huyo, Mizengo Pinda kumuingilia katika utekelezaji wa majukumu ya wizara yake.

Vyanzo vimefafanua kuwa uamuzi huo umesababishwa zaidi na matukio ya hivi karibuni ya Pinda kukosoa hadharani kazi ya bomoa bomoa kwenye hifadhi ya barabara lililokuwa likitekelezwa na waziri huyo na kuagiza lisitishwe hadi hapo itakapo amuliwa vinginevyo na Baraza la Mawaziri.
JE NI KWELI?

Thursday, March 17, 2011

E.A. WATATAKIWA KUUNGANISHA NGUVU ILI KUTOKOMEZA UGONJWA WA UKIMWI

Nchi zilizo wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki zimetakiwa kuendeleza ushirikiano kwa ajili ya kubambana na janga la maambukizi ya ugonjwa unaosababisha virusi vya ukimwi na baadaye kupata ufumbuzi wa tatizo hilo ambalo limeteketeza nguvu kazi miongoni mwa jamii ya nchi hizo. Hayo yalisemwa na Dk. Fatuma Mrisho, ambaye ni Mwenyekiti Mtendaji wa Tume ya Kuthibiti Ukimwi nchini Tanzania, wakati akitoa hotuba yake ya ufunguzi wa mkutano wa siku tatu wa wadau walio katika mapambano dhidi ya maambukizi ya ugonjwa wa ukimwi kutoka nchi zilizo katika jumuiya hiyo ambazo ni Kenya, Uganda, Tanzania, Rwanda na Burundi ambao uliofanyika katika hoteli ya Nyumbani jijini Mwanza.

Amesema kuwa mikakati iliyopo kwa sasa ya kupambana na maambukizi ya ugonjwa wa ukimwi, ni nchi zilizo katika jumuiya hiyo kuendeleza mipango ya kutokomeza tatizo hilo kwa ushirikiano wa karibu kwa nchi zilizo mwanachama ambazo ni Kenya, Uganda, Tanzania, Rwanda na Burundi kwa kutoa semina, kongamano na mbinu zingine ambazo zitaweza kuwaelimisha wananchi ili kubadirisha tabia zao ambazo zinaleteleza maambukizo ya ugonjwa huo.

Dk. Mrisho amesema kuwa maambukizo mengi katika miongoni mwa wananchi walio katika Jumuiya hiyo yanatokana na ngono zembe miongoni mwa jamii, madereva wa magari makubwa yanayosafirisha bidhaa baina ya nchi hizo, wafanyakazi katika mabaa na sehemu zingine za starehe pamoja na maeneo yenye mlundikano wa watu wengi ambao huleteleza muingiliano usio rasmi.

Ameongeza kuwa endapo nchi zilizo katika Jumuiya ya Afrika Mashariki zitafanya kazi kwa pamoja katika kutokomeza janga hilo, hadi kufikia mwishoni mwaka 2012, ugonjwa huo utakuwa umetokomezwa kabisa au kupungua kwa kiasi fulani iwapo jamii katika nchi husika itajikita katika kuthibiti maambukizo hayo.

Hata hivyo, Dk. Mrisho amesema kuwa nchi zilizo katika jumuiya hiyo kwa kupitia taasisi zilizo katika mapambano dhidi ya ugonjwa huo zitakutana mara kwa mara ili kubadirishana uzoefu wao, itakuwa ni rahisi kutambua matatizo yaliyo katika nchi husika na kuweza kushirikiana katika kuyatatua ili kuweza kuwa na malengo ya pamoja katika kubambana na ugonjwa huo.

Mkutano huo ambao umeanza Machi 16 utahitimishwa kesho Machi, 18 ambapo kwa mujibu wa Dk. Mrisho ambaye ni mwenyeji katika mkutano huo, wajumbe wataweza kutoa maamuzi ya jumla ambayo yatalenga kutokomeza maambukizi ya ugonjwa huo.

HAPA NA PALE A- TOWN

Moja kati ya vielelezo kamilifu vya mkoa wa Arusha (ukiona chata hii basi ujue ni A town kwani haipatikani kwingine kokote kule duniani zaidi ya hapa).

Sheikh Amri Abeid Stadium kwenye kona hivi kwa nje nyuma ya ubao panapoandikwa magoli.

Kilombero sokoni.

Tembo katikati ya mji.

Kuelekea shule ya msingi na ufundi Kaloleni.

MSAFIRI KARIRI

Madereva wa pikipiki nchini Pakistan ni mafundi kwelikweli linapokuja suala la kusaidia mteja kuminimaizi cost za maisha, Hebu cheki na picha hii iliyopigwa katika barabara kuu nchini humo.

Mbona patatosha tuu...!

Wednesday, March 16, 2011

WIKI YA MAJI YAZINDULIWA LEO JIJINI MWANZA.

Waziri wa Maji,Prof. Mark Mwandosya (kulia) pamoja na Mkuu wa Jumuia ya Ulaya Nchini Balozi,Tom Clarke (pili kushoto) wakimsikiliza kwa makini mwandisi mshauri wa maradi wa maji taka katika eneo la Butuja alipokuwa akitoa maelezo ya mradi huo leo jijini Mwanza.

Waziri Wa Maji Mh. Mark Mwandosya leo amefungua wiki ya Maji mjini hapa kwa kuzindua mradi mkubwa wa Maji taka katika eneo la Butuja Wilayani Ilemela Mwanza.

Akitoa taarifa ya utekelezaji wa Mradi huo, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka Mwanza (MWAUASA) Bw. Mashaka Sitta alisema kuwa mradi huo utakaogharimu karibu Billioni 29 ulibuniwa mwaka 2002 na kuanza kutekelezwa tangu mwaka 2009.Alieleza kuwa miradi itakayojumuisha katika mradi huo ni pamoja na ujenzi wa bomba kubwa la kipenyo cha mm 700 kwa umbali wa mita 140,ujenzi wa mabwawa mapya matatu, ukarabati wa mabwawa kumi ya zamani, ujenzi wa matanki mapya ya kuhifadhia Maji taka pamoja na ununuzi wa vifaa vya maabara.

‘’ Tunatarajia kuwa kukamilika kwa mradi huu itatuwezesha kujenga pia mtandao wa Maji taka kwa kilomota 24, kujenga mashimo ya maji taka (manhole chambers) zipatazo 880 itakayounganisha karibu nyumba 5000 kwenye mtandao wa majitaka’’ alisema Mkurugenzi huyo.


Akizungumza baada ya uzinduzi huo, Mh Waziri alisisitiza umuhimu wa kutunza miradi hii kwani Wafadhili wanatumia fedha nyingi kugharamia miradi hii. ‘’Nisingependa baada ya ufunguzi huu wa leo, tuwaombe tena Wafadhili kutukarabatia miundominu yetu nitashukuru kama kutakuwa na kazi ya mamna hii katika Nchi moja ya jirani basi kazi hiyo ifanywe na MWAUSA’’ alisisitiza Mwandosya.

Pamoja na uzinduzi huo Mh.Waziri alipokea pia magari 4 ya kubebea maji taka yatakayotumika na Mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka jiji Mwanza.Sherehe ya UzinduzI wa mradi huu mkubwa maji taka ulihudhuriwa pia na Mwakilishi mkuu wa Jumiya ya Ulaya hapa Tanzania Balozi Tom Clarke, Balozi Mdojo wa Ujerumani hapa Nchini pamoja na Mkurugenzi Mkazi wa Benki ya maendeleo ya Ujerumaini (KWF) Dr Wolfgang.

Maadhimisho ya wiki ya Maji yanafanyika katika viwanja vya Nyamagana jijini Mwanza na yatafikia kilele chake tarehe 22 Machi kwa kufungwa rasmi na Makamu wa Raisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Gharib Bilal.

ASKOFU ALPHA FRANCIS MOHAMED AAGWA LEO MJINI ARUSHA.

Ibada ya kuuaga mwili wa Askofu Alpha Francis Mohamed Imefanyika leo katika kanisa la anglikana Arusha Christ Church Cathedral Diocese of Mountain Kilimanjaro.

Jaji mkuu mstaafu Barnabas Samata akitoa heshima zake za mwisho kwa mwili wa marehemu baba askofu Alpha Francis Mohamed.

Mchungaji Kajembe akitoa heshima zake za mwisho kwa mwili wa baba askofu.

Askofu Alpha alikuwa ni mmoja wa waanzilishi wa dayosisi ya mtakatifu Kilimanjaro, na katika maisha yake amevisaidia vikundi mbalimbali vya akina mama katika kuanzisha miradi na kuwezesha kusomesha watu mbalimbali.

Muimbaji wa muziki wa injili Betrice Muhone ni mmoja wa waliohudhuria ibada hiyo.

Kwaya ya Upendo kutoka st.James Arusha katika heshima za mwisho.

Mungu wa rehema nyingi, Baba wa Bwana Yesu kristo uliye ufufuo na uzima, ambaye kila amwaminiye yeye, ajapokufa, ataishi, na kila mwenye kuishi ndani yake na kumwamini hafi milele.

Watumishi wa mungu katika picha ya pamoja na mwili wa marehemu baba askofu Alpha Francis Mohamed aliye zaliwa tarehe 22/nov/1941 na kufariki dunia tarehe 14/march/2011, Mwili wake umesafirishwa leo kwa ndege ya Precision air kuelekea mkoani singida kwa mazishi. Bwana ametoa na Bwana ametwaa jina la Bwana lihimidiwe.

Tuesday, March 15, 2011

KOSHA MACHO NA VINYAGO VYA KWETU...

Niko nje kidogo ya mji wa Arusha panaitwa Manyara kibaoni, barabara kuelekea Serena Lodge Hotel nakutana na banda la bidhaa za jadi kilizotengenezwa kwaajili ya mapambo kwa nyumba.

Ni zaidi ya ubunifu kwa sanaa za mkono zilizopo katika duka hili.

Viatu vya jadi maray'yo aka makatambuga na marimba.

Sanaa.

Picha za ukutani..

Part two.

Zana asili zilizotumika toka makabila ya wamang'ati, wamasai na wameru nazo zinauzwa hapa.

Ni nyenzo nyingi za bidhaa asili zinapatikana hapa.

TAHADHARI KWENYE MTAMBO WA NYUKLIA JAPAN.

Fundi mitambo wanahangaika kudhibiti kinu cha tatu cha kinyuklia katika mtambo wa nyuklia kilichokumbwa na tetemeko kubwa la ardhi, ambalo limetikiswa na mlipuko wa pili katika kipindi cha siku tatu. Vyuma vya mafuta vilivyopo ndani ya kinu hicho kwenye mtambo wa Fukushima Daiichi vimefunuliwa katika nyakati mbili tofauti, na kuzua wasiwasi wa kuyeyuka. Maji ya baharini yamekuwa yakitiwa kwenye kinu hicho ili kuzuia kupashika joto kupita kiasi.

Moja kati ya boti za starehe ilikutwa juu ya ghorofa katikati ya mji wa Otsuchi mara baada ya dhahama lililotokea hivi majuzi. Kushindwa kufanya kazi kwa mfumo wa kupunguza joto kulianza kabla ya milipuko kutokea kwenye mtambo namba 3 na mtambo namba 1 siku ya Jumamosi

Uharibifu kwa barabara.
Mlipuko uliotokea hivi karibuni ulijeruhi watu 11, na mmoja ameumia sana.

Mlipuko huo ulitikisa umbali wa kilomita 40 kutoka ulipotokea na kusababisha moshi mkubwa hewani. Jengo lililokuwa nje ya mtambo huo uliharibika sana.