ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Monday, December 5, 2011

HATIMAYE MR EBBO AZIKWA NYUMBANI KWAO

Askofu Thomas Laizer akiongoza sala katika safari ya mwisho ya Mr. Ebbo mjini Arusha.

Dada wa marehemu akitoa heshima za mwisho kwa mwili wa marehemu Mr. Ebbo.

Familia ya Mr.Eboo.

Maelfu ya wananchi wamejitokeza kwa wingi leo mjini Arusha katika safari ya mwisho ya msanii wa muziki wa kizazi kipya (bongo flava)Abeili Motika almaarufu kwa jina la Mr.Eboo ambaye amezikwa kwenye makaburi ya ukoo nyumbani kwa mzee Lotiko.

Wananchi hao ambao walikuwa na shauku ya kuuaga mwili wa marehemu huyo walijitokeza kwa wingi huku wakionekana kuwa na nyuso za majonzi, kila mmoja akihuzunika na wengi wakidai kuwa mwimbaji huyo wa bongo flava ameacha pigo kubwa kwa jamii ya kimasai na Taifa kwa ujumla kwani muziki wake sambamba na kuburudisha ulikuwa unaelimisha kwa kiwango kikubwa.

Akiongea katika mazishi hayo askofu mkuu wa jimbo la kaskazini Thomas Laizer alisema kuwa wao kama kanisa wameupokea msiba huo kwa masikitikio makubwa kwani msanii huyo alikuwa anaelimisha jamii kupitia nyimbo zake pia aliweza kuutangaza mkoa wa Arusha pamoja na thaminisha asili ya kabila la kimasai kupitia nyimbo zake.

Tupe maoni yako

2 comments:

  1. inalillah wainalilahh rajeun

    ReplyDelete
  2. I am a LUO who grew up as a Bantu Tribe, My Identity was Changed, I personally will miss Ebbo; Education and fun..The only 1 we had.. Yusuf Musoke..Uganda

    ReplyDelete

Note: Only a member of this blog may post a comment.