ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, November 25, 2011

TWANGA PEPETA WAKWEA PIPA 2 LONDON UK.

Twanga Pepeta ''KISIMA CHA BURUDANI'' wameondoka leo asubuhi kutoka uwanja wa kimataifa wa Julius Nyerere kuelekea kuvinjari katika Jiji la London ili kusugua kisigino na wapenzi wao walioko nchini Uingereza na nchi jirani ikiwa ni katika kusherehekea maadhimisho ya Miaka 50 ya Uhuru wa Tanzania.Bendi ya Twanga Pepeta wakijiandaa kuingia kwenye Pipa

Chalz baba akiwa tayari kuingia kwenye Pipa

Full Mzuka

kikosi cha Twanga kikijiaandaa kuingia Katika Uwanja wa Julius Nyerere

Kutoka Kulia Amigolous akiwapa Mikoba Jojoo, Jumanne, Baby Tall na Luiza

kutoka kushoto Shalapova, Charles Baba na Shakashia

Victor Mkambi mpiga kinanda wa Twanga akiwa na Maria Soloma ambae ni dancer wa twanga

MPANGO MZIMA:-
Kundi hilo lililokamilika katika safu zake za waimbaji, wapiga vyombo na wacheza show linatarajiwa kuwasha moto wa burudani yao siku ya Jumamosi, tarehe 26 Novemba 2011 katika Ukumbi wa Club 2000 Savoir Banqueting Suite, Popin Building Southway, Wembley HA9 0HB kuanzia saa Tatu Kamili Usiku mpaka alfajiri (9pm til late).

Mheshimiwa Balozi Peter Kalaghe atakuwa mgeni rasmi. CD za album mpya na za zamani zitauzwa na vinywaji pamoja na vyakula vya kitanzania vitakuwepo vya kumwaga. Viingilio vitakuwa £20 (singles) na £35 (couples) kabla ya saa sita (mid night) na £25 (singles) na £40 (couples) baada ya saa sita usiku.

Njoo tujumuike, njoo usugue kisigino, njoo usherehekee uhuru wa nchi yako, njoo ule na kunywa kitanzania. Burudani ni watu na watu ni pamoja na wewe. Tanzania itajengwa na watu wenye moyo kama wewe. Karibuni sana.

Shughuli hii imeandaliwa na Urban Pulse Creative wakishirikiana na Miss Jestina Blog, chini ya maelekezo thabiti ya Ubalozi wa Tanzania, London.

Tumethubutu, Tumeweza na Tunazidi kusonga Mbele

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.