ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Tuesday, November 8, 2011

SHEREHE ZA SIKU YA KUZALIWA MWANZAILISHI WA DINI YA SIKH GURU NANAK

Maelfu ya wafuasi wa dini ya Sikh walijitokeza siku ya Jumapili tarehe 6 Novemba 2011 katika mjini wa Southall, Middlesex UK ili kusherekea siku ya kuzaliwa kwa mwanzilishi wa dini yao Guru Nanak aliezaliwa mwaka 1469 nchini Pakistani.Waumini wa dini ya Sikh wakiazimisha siku hii..

Halaiki ya kubwa ya waumini wa dini ya Sikh wakisherekea

Wadau wakiwa kazini kutayarisha chakula.

Hata watoto nao walikuja kusaidia kutayarisha chakula

Wakati wa kupata mapocho pocho.

chakula kilikuwa bure kwa kila mtu

Frank wa Urban Pulse ni mmoja wa mashuhuda hapa akiwa katikati ya mitaa ya Southall kushuhudia sherehe hii.

Muasisi wa Dini ya Sikh Guru Nanak.

Inatajwa kuwa wakati akiwa na umri wa miaka 30 alipotea kwa hali ya miujiza kwa mda wa siku tatu. Alipo rejea alianza kuhubiri, kufundisha na kuandika dini ya Sikh wakati maisha yake yote. Pia Guru Nanak alisafiri dunia nzima kuitangaza na kujadili dini hii kwa waumini wengine kama waislamu pamoja na Hindus

Kwa Miaka zaidi 550 wafuasi wa dini hii wamekua na desturi hii ya kusherekea siku moja kabla ya kuzaliwa kwake Guru Nanak kwa kuandaa maandamano haya makubwa ya Sherehe hii ambayo hufanyika India pamoja na baadhi ya sehemu za nchi ya Uingereza. Kwa kawaida sherehe hizi huongozwa na wafuasi wakuu watano wanaojulikana kama ''Panj Piare'' wakiambatana waimbaji, wanamuziki na timu ya wacheza upanga (Martial Arts) kuelekea hekaluni kwao ''Gurdwara'' Sri Guru Singh Sabha, hapa Southall hekalu lao ndio kubwa kuliko yote katika bara la ulaya.

Sherehe hizi huanza mapema asubuhi kwa kuimba, kuomba kwa pamoja. Baadae chakula cha kitamaduni kinachojulikana kama ''Langar'' hutolewa bure kwa kila mtu.

Maandamano ya Southall yanaitwa Nagar Kirtan,

CHANZO NA URBAN PULSE CREATIVE.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.