ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, November 4, 2011

MAFUNZO YA TACAIDS KWA WAANDAAJI NA WATANGAZAJI YAMALIZIKA LEO MWANZA

Watoa mada Glory Mziray na Richard Ngaiza wakifuatilia hatua ya mwisho ya mafunzo hayo ya siku mbili inayohusu Kubainisha changamoto zinazo ikabili sekta ya upashaji habari kwa vipindi vya elimu ya Ukimwi kwa redio, kwenye semina hiyo inayotolewa na TACAIDS.

Kwa siku ya leo washiriki walijigawa kwa makundi kulingana na mikoa kukusanya changamoto zao na kuzipima ambapo baadaye waliziwasilisha zikiwa na either utatuzi au ushauri. Pichani washiriki kutoka mkoani Shinyanga.

Washiriki wa redio mbalimbali za kijamii kutoka jiji linalokuwa kwa kasi, uchumi wake ukiendeshwa na biashara kubwa ya samaki na spidi kali ya ongezeko la watu Mwanza, Uzoefu unaonyesha kuwa mwingiliano wa watu kutoka sehemu na sehemu ni chanzo cha ongezeko la maambukizi ya ukimwi.

Mara ni miongoni mwa mikoa yenye makabila mengi nchini Tanzania, mila inachukuwa nafasi kwenye maisha ya wakazi wa maeneo hayo na kuegemewa na wengi, takwimu zinaonyesha kuwa baadhi ya mila zilizopo zinahusika katika kuchangia maambukizi.

Mkoani Kagera ambako inasemekana kwa upande wa Tz ndipo ulipoanzia, takwimu zinaonyesha ugonjwa huo unazidi kupungua kiasi cha asilimia 3.4 lakini kuna tabia na mienendo inayoonyesha kuwa hali ya baadaye itakuwa mbaya iwapo hatua za dhati hazitochukuliwa.

Kwa mwingiliano wa kibiashara na wakimbizi mipakani mwa nchi nako hali si shwari maambukizi ni ya kasi watu wakiamini hadithi za mitaani zaidi kutokana na uhaba wa elimu stahiki kuhusu Ukwimwi, by washiriki toka Radio Ekwizera.

Uwasilishaji pia ulikuwa na kipengere cha Je! Tunapimaje Mwitikio wa wasikilizaji aka Je! Tunasikilizwa na Tutatambuaje kama vipindi vya ukimwi virushwavyo na kituo husika vinasikilizwa na vinamanufaa kwa jamii??

Produser maarufu hapa nchini Duke, alikuwa bize katika meza yake akikusanya sauti ya yote yaliyokuwa yakijiri kwenye mafunzo hayo toka Tume ya kuthibiti ukimwi nchini (TACAIDS) chini ya usimamizi thabiti wa Kampuni ya Masoko AGENCIES (T)Ltd.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.