ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Tuesday, October 4, 2011

MTIHANI WA KIDATO CHA PILI WAREJESHWA.

WAKATI jana wanafunzi wa kidato cha nne wakianza mitihani yao ya kuhitimu elimu ya sekondari, hatimaye serikali imerejesha tena mtihani wa kidato cha pili.

Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Philip Mullugo, alitangaza urejeshaji huo mbele ya wananchi wa jimbo lake la Songwe lililoko wilayani Chunya, mkoani Mbeya.

Mullugo alisema kuwa ili kupunguza kushuka viwango vya ufaulu hapa nchini hasa kwa kidato cha nne, serikali imeamua kurejesha mtihani huo wa kidato cha pili na wanafunzi wote watatakiwa kufikisha wastani wa alama 25 ili kuendelea na masomo ya kidato cha tatu.

“Kuanzia mwaka huu hakuna mwanafunzi atakayeruhusiwa kuendelea na kidadto cha tatu bila kufanya mtihani wa kidato cha pili na kufikisha wastani wa 25,” alisema Mullugo.

Wakati huohuo, Naibu Waziri huyo wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi alitoa msaada wa zaidi ya shilingi mil. 277 kwa ajili ya kusaidia elimu jimboni humo.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.