ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, September 16, 2011

ZAIDI YA WANANCHI 100 KISEKE JIJINI MWANZA WAVUNJIWA MAKAZI YAO, ZOEZI LAFANYIKA CHINI YA AMRI YA MWENYEKITI

Zaidi ya wakazi 100 wa MTAA WA MIEMBE GIZA – KATIKA MLIMA WA KISEKE WILAYANI ILEMELA JIJINI MWANZA WAMEAPA KUTOHAMA KATIKA ENEO HILO KUTOKANA NA MWENYEKITI WA MTAA WA MIEMBE GIZA BWANA KAMANI KUVUNJA MISINGI YA NYUMBA 35 NA NYUMBA ZAIDI YA 100 WALIZOKUWA WAMEJENGA HIVYO KUWASABABISHIA HASARA NA UPOTEVU WA MALI ILE HALI BAADHI YA NYUMBA WANAZODAI KUWA NI ZA MATAJIRI ZIKIBAKIA KATIKA ENEO HILO BILA KUVUNJWA.

Wakizungumza na blogu hii katika eneo la tukio wananchi hao wamesema kuwa mnamo mwezi September 3 mwaka huu majira ya saa 10.30 jioni Mwenyekiti wa mtaa huo bwana Kamani akiongozana na watu wake kwa kutumia nguvu alibomoa nyumba na misingi ya nyumba za wakazi hao hali ambayo wanadai ni makosa na haikuwa sahihi.

Kupitia amri ya mwenyekiti wa kitongoji hicho nyumba nyingi zimebomolewa, mali kuharibiwa na nyingine kupora huku baadhi ya wakazi wa eneo hilo wakiachwa hawana mahala pa kujisitiri.

Babu Ntambi moja kati ya waliovunjiwa ameapa kutoliachia eneo lake kwani limemgharimu zaidi ya shilingi milioni 11 kulisawazisha na hatimaye kupata kiwanja ambacho alianza kujenga nyumba ambayo hata hivyo imebomolewa.

Ilikupata kiwanja imlibidi kusawazisha eneo kwa mawe na kujaza udongo kama inavyoonekana.

Wananchi hao wamehoji kuwa kama kweli eneo hilo limetengwa kwaajili ya hifadhi iweje zoezi hilo lifanyike kwa baadhi ya nyumba ile hali likiruka nyumba za marafiki wanaotajwa kuwa ni wa mwenyekiti waliogawiwa na kiongozi huyo maeneo.

Kwa upande wake Afisa ardhi wa jiji la Mwanza bw. Makusudi Bwabo amesema kuwa nyumba hizo zilizojengwa ndani ya hifadhi ya mlima huo wa Kiseke zimejengwa kimakosa kwa madai kuwa mlima huo umetengwa kisheria na uongozi wa jiji kwaajili ya hifadhi ya msitu na kwamba wale wote waliojenga kwenye msitu huo ni wavamizi hiyo ni kwa mujibu wa sheria ya mipango miji ya mwaka 2007 kifungu namba 8 na hatua inayofuata ni kubomoa nyumba zao.

Wakati yote hayo yakiendelea ndiyo kwaaanza ujenzi unaendelea tena baadhi ya wananchi wenye fedha wakijitengenezea viwanja kwa kuumega mlima huo.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.