ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, August 10, 2011

ANATAFUTWA NA MWAJIRI WAKE

Jamaa anaye tambulika kwa jina la Juma Hemed Hamisi (pichani)anatafutwa na Jeshi la polisi mara baada ya kutoweka na kiasi cha pesa shilingi za kenya 115,000/= (lakimoja kumi na tano elfu) sawa na shilingi za Tanzania 2,127,500/= (milioni mbili lakimoja na ishirini na saba elfu na miatano), pamoja na pesa taslimu za kitanzania shilingi laki tatu alizokabidhiwa kwaajili ya kufanya malipo mbalimbali.

Dreva Juma Hemed Hamisi inatajwa kuwa alipofika mpakani aliliitelekeza gari hilo lenye namba za usajili T106 ABQ roli aina ya Scania mali ya Lakairo Investiment likiwa na mizigo yake, akitokea nchini Kenya kuingia Tanzania.


Taarifa za tukio la kutoweka kusiko julikana kwa dreva huyo huku akiwa na mafungu ya watu yaani jumla ya fedha ikiwa ni shilingi milioni mbili laki nne ishirini na saba na mia tano, akimwacha mwajiri wake mdomo wazi asijuwe kisa na mkasa tayari zimeripotiwa kwa jeshi la polisi kupitia RB no MZN/RB/5347/11.

Roli lililotelekezwa tayari limekwisha fikishwa kwa mwenye mali mara baada ya dereva mwingine kuagizwa kulifuata mpakani. pichani likiwa kwenye karakana ya Lakairo Investiment, Mwaloni Kirumba jijini Mwanza

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.