ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, June 10, 2011

MDAU ANENA TOKA UJERUMANI....

I know you have travelled the world and this might not really be of any interest, but to me a first timer, felt to share with you some experiences of while in Europe. I am officially destined to Germany but have had the opportunity to travel to neighbouring countries Holland and Denamark. Joseph Sekiku akiwa mpakani mwa Ujerumani na Denmark.
1. The borders are entirely free (hakuna cha afisa uhamiaji, hakuna cha polisi, hakuna cha passipoti, hakuna chochote). Labda vibao vinavyokuonyesha ..sasa unaingia mfano Uholanzi, au Denmark au Ujerumani.


Nikiwa katika ziara hii nimejiuliza maswali mengi.. sisi africa kuna nini? Hata baada ya kuwapo na umoja wa afrika mashariki, kitabu cha pasipoti hujaa mihuri, ukifika katika mipaka yetu, belia kibao.


Nakumbuka kwetu Karagwe (mkoa wa kagera) kwenda Uganda: Unapofika Kyaka kuna belia, na unapofika Mtukula, niliacha belia 3 upande wa Tanzania, na kuingia Uganda, kuna belia 2. Impression ya kwanza, ni kama unapokwenda hapaendeki. Tofauti ambayo nimeiona tuu denmark, wao wanatumia DK Kronners ingawa wamepokea Euro niliponunua chakula katika mgahawa. Hivyo nakutumia picha chache.

Wind turbine kwa ajili ya umeme wa upepo.
2. Nishati: Ninaposikia sakata la umeme nchini kwetu, najiuliza maswali mengi? Mbona huku ulaya wanazima mitambo yao ya kufufua umeme na kuwekeza katika nishati endelevu ya upepo na umeme wa jua?

Solar panel katika majengo
Kwa nini TANESCO au SERIKALI (wizara husika) isiwekeze katika umeme kama huu wa jua au upepo. Nikiangalia tuna bahari na coastline ndefu sana. Je tungeliwekeza katika umeme wa upepo, tusingepata umeme mwingi? Mbona hawa wameweza jamani? Nakuletea picha hizi chache uone huku wanavyoweza...

Inverter za kubadilisha umeme sola kuwa umeme wa AC
Sisi mara Richmondi, mara Songeshaz' mara nini,... hatutafika popote. Jua tunalo la kutosha, upepo tunao wakutosha.

Meli hiyoooo
3. Miundo mbinu: Natoka mkoa wa Kagera na usafiri wa maji tulionao umebaki meli moja tu ya Mv Victoria, ambayo imesafiri katika ziwa hili kwa zaidi ya miaka 40? Na juzi nimetembelea mji wa Panerbug ilipotengenezwa meli ya MV Liemba iliyoko katika mji wa Kigoma, nikakuta sasa wao wameisha fikia uwezo wa kutengeneza meli kubwa sana duniani. Nakuletea picha hapa Angalia meli hiyo ukubwa wake.

Barabara chini ya Ardhi
4. Miundo mbinu, usiseme. Na kwa upande wa barabara, nilikuwa najiuliza ili kasumba na tararatibu za BOMOA BOMOA, nimejiuliza nikasema kuwa, kama watu tayari wanaishi katika mazingira, na sasa unataka kutengeneza barabara, kwa nini barabara hiyo isipite katika maeneo ambayo hayana makazi? si lazima kusumbua utarataibu na makazi ya watu. Barabara kuu inarahisisha uchukuzi.. si miji hata ikibaki pembeni, inaweza kuunganika na barabara kuu kuliko, kubomoa nyumba za watu, n.k?

Samahani kaka kwani picha ni nyingi kidogo na labda hauna bandwidth ya kutosha.


Wako,

Joseph Sekiku
Ujerumani

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.