ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, June 10, 2011

WATUMIAJI WA BIA NA SIGARA HAWAHITAJI BAJETI

Mtangazaji mahiri wa Star Tv Yahaya Mohamed (kushoto) akiongoza mada ndani ya kipindi cha asubuhi Tuongee, pembeni yake ni Bw. Mohamed Moledina Mfanyabiashara, Diwani mstaafu na mwanahabari Albert G. Sengo.

Utashi wa viongozi, uwezo duni wa wasimamizi, viongozi kujali maslahi binafsi na kuweka kando maslahi ya Umma ni moja kati ya mambo yaliyojitokeza na kutiliwa mkazo leo hii kwenye kipindi cha 'Tuongee Asubuhi' kupitia Star Tv ambapo mada kuu ilikuwa ni kuijadili Hotuba ya Bajeti ya Serikali ya Mwaka 2011/2012 iliyotolewa jumatano (trh 8 juni) na waziri wa fedha na Uchumi Bw. mustapha Mkulo.

Safari mezani.
Nimefurahishwa na sms nilizokutana nazo kwenye simu yangu moja ikisema 'Pombe, sigara na mvinyo hata vikipanda kwa asilimia ngapi, kiwango chochote mimi na wanywaji wenzangu tutaendelea kunywa tu hadi kieleweke kwani wanywaji hawana bajeti'

Tangu enzi za hayati Mwalimu Julius K.Nyerere wakati huo bia ikiuzwa Tshs 50 kwa chupa hadi leo awamu ya nne ya Jakaya ambapo chupa moja inauzwa kuanzia Tshs. 1,500 katika baa za kawaida hadi Tshs. 3,000 kwenye mahoteli makubwa watumiaji wanakunywa kwa kiwango kilekile na zaidi na zaidi wengine maelfu na makumi matatu wakiongezeka na wala hatujashuhudia watu wakiandamana kudai haki ya punguzo.

Mtunza bustani akiwa bize kuihudumia moja ya engo za bustani ya makao ya Sahara Communication Mwanza.

TAKWIMU ZA BAJETI:
Mfumuko wa bei hadi April 2011......8.6%
Pato la Mwananchi hadi 2010..........sh.770,463
Akiba ya Dola hadi desemba 2010.....$milioni 3,948
Ukuaji wa uchumi mwaka 2010.........7%
Riba katika mabenki mwaka 2009......13.4%
Shilingi kuporomoka mwaka 2009......8.5%
Thamani ya Shilingi kwa dola ...........$1=1432
Uuzaji biashara nje umekuwa 2009....24%
Akaunti katika mabenki...................4,241,610
Matawi ya benki nchini yamefikia.......475
ATM nchi nzima zimefikia.................966
Mapato ya ndani (2010)yameongezeka..8.7%
Deni la Taifa limekuwa hadi..............$millioni 11,380
Nguvu kazi ya Taifa 22,661,280.........52.7%
Wenye ajira milioni 8......................35.3%

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.