ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, May 11, 2011

WHAT NEXT AFTER KIKOMBE CHA BABU?

Babu anakula vichwa like crazy.

Tangu habari za “Babu” wa Loliondo ziingie mitaani, mchungaji mstaafu huyu Ambilikile Mwasapila amekuwa akipata wateja wa kumwaga na waliopo kwenye “waiting list” yake si chini ya 25,000.

Mtaalamu huyu wa miti shamba anaaminika kuwa na “magical cure” kwa magonjwa yote sugu ikiwa ni pamoja na gonjwa la UKIMWI. Sijajua kwa hakika ni kiasi gani anauza dawa zake ila kwa kifupi babu huyu kama hakika dawa zake zinatibu pumu, kisukari, ukimwi n.k basi once foleni inapungua huko Loliondo blog hii itamtafutia sponsors na kumleta kiwanja kufanya kweli.
Ni wakati muafaka wa serikali ya Tanzania kuangalia na kufanya utafiti wa hali ya juu kuhusu dawa za retired pastor huyu ili kumuweka kwenye mazingira mazuri ya kufanya kazi yake ya kutibu watu.Taifa linajengwa na watu wenye afya njema,just tazama viongozi wangapi wa serikali waliokwenda Loliondo kupata tiba.

Formula yake inaweza kuwa ni big deal internationally na kuiweka Tanzania kwenye ramani ya moja ya nchi zenye watafiti wa hali ya juu,japo ni ishu ya miti shamba.Nina imani babu huyu na dawa zake ni msaada mkubwa kwa watanzania.Who would have thought tiba ya “ngoma” itagunduliwa na mtanzania?

Ngorongoro hapaingiliki sasa maana kuna foleni kubwa ya magari yenye wagonjwa na wateja wanaosubiri huduma za Mchungaji Ambilikile. Watu toka kona zote za Tanzania plus Kenya na Uganda wanamiminika Loliondo kila kukicha.Big up to “Babu” Ambilikile kwa kuja na tiba hizi.


By tunyfish.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.