ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, April 20, 2011

SHERIA NA KANUNI ZA SERENGETI FIESTA SOKA BONANZA MWANZA ZAWEKWA HADHARANI.

Leo majira ya saa tano asubuhi viongozi wa timu za mashabiki wa soka la ulaya kwa timu za Real Madrid, Arsenal, Man U, Liverpool, Inter Milan, Ac Milan, Chelsea na Barcelona wamekutana na kamati ya maandalizi ya bonanza hilo kwa nia ya kupeana kanuni na taratibu mbalimbali juu ya uchezeshwaji wa ligi hiyo.

Ligi ya Serengeti Fiesta Soka Bonanza inatarajiwa kufanyika jumamosi hii ya tarehe 23 April 2011 katika viwanja vya CCM Kirumba jijini Mwanza kuanzia saa 4 asubuhi na kuendelea hatimaye kumpata bingwa.

Akizungumza mbele ya Marais wa timu hizo za Mashabiki mratibu mkuu wa Bonanza hilo Shafi Dauda amesema kuwa kanuni zitakazo tumika ni kama ifuatavyo:
1. Timu kila timu inapaswa kusajili wachezaji 15 tu, kati yao kila timu itasajili wanawake wa 3.
2. Kila timu mwisho kusajili wachezaji wa 2 wa ligi kuu (ambao si lazima)
3. Mchezo utachezwa kwa dakika 20 (kumi kumi kwa kila kipindi) na dakika 2 za mapumziko.
4. Substution ni kadri uwezavyo.
5. Hakuna offside
6. Timu zitacheza Wachezaji saba kila upande akiwemo golikipa.
7. Mchezo ukichezwa na ikipatikana draw zitapigwa penati tatu, tatu na kuamua mshindi na ikishindikana kumpata mshindi utaratibu wa moja moja utachukuwa nafasi.

8. Timu mbili au tatu zikifungana :
A Pointi nyingi ndiye atakaye pita
B Kanuni ya tofauti ya magoli kuzingatiwa.
C Zilipo kutana wenyewe kwa wenyewe nani alimfunga mwenzie.

Bonanza hilo litatanguliwa na maandamano majira ya saa 2 asubuhi yatakayoanzia Uwanja wa Njamagana hadi Uwanja wa tukio CCM Kirumba.
Wadhamini: Serengeti premium lager, Isamilo hotel, club lips, Star max hotel, Malaika hotel, Nyumbani Hotels na G&G hotel.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.