ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Monday, April 18, 2011

KISESA YAZINDUKA KISAWASAWA!!!....

Jana jioni kijiji cha Kisesa wilaya ya Magu, mkoa wa Mwanza kulikuwa na show safi yamtakato ya muziki wa kizazi kipya iliyofanyika kuhamasisha utumiaji wa vyandarua na vita dhidi ya maralia. ZINDUKA.Fid Q. alikuwa ndiye rais wa mpango huo nae alishiriki vilivyo kutoa elimu sambamba na kutoa burudani kwa hadhira. Duh hadi watoto wanazikwachu songi zake!!

Eh bana Mpango wa Zinduka umetuletea mengi kwani kuna vichwa vya ukweli vimejificha kitaa na hii ilikuwa fursa kuona kwaliti zao kama Mc huyu aitwe D-Malick' wa RNB na wimbo 'Mtima wange' ni nowmaaa mazee!

Mtoto atumwi dukani-Ingawaje Show hiyo iliingiliwa na mvua kubwa katikati wakati ndo ngoma imenoga, baadaye mvua hiyo ilikoma na utamu kuendelea...

Kwakila ambacho Fid Q. alikuwa akiwaomba mashabiki kufanya hawakumwangusha....!!

Jitah man aka Zagamba wenye roho mbaya lazima waisome namba akikamua...

Amini usiamini huyu ni babu wa miaka 62 jukwaani, aliwaacha hoi wananchi kwa kuzikamata fresh swaga za ki-hip hop, akinata na beat kwa mashairi makali...
Shangwe wacha zilipuke kwa babu!!!!Namuna hiii.

AAaaah! Wacha Babu awe *Star* cheki kwenye snepu Watangazaji Philbert Kabago wa Passion Fm (shoto) na Ezden (kiss Fm).

Adja-dja-dja- Pale katii bonge la 'mmechisho'

Toka rock city wasanii lebo ya Mo-records kwa producer Q.The Don pichani kutoka shoto ni X-lady, B-snicker na Zombi.

Kabla ya burudani hiyo . Balozi wa malaria Fid Q alitembelea nyumba kwa nyumba kukagua, kuangalia na kuona kama kaya jeh! zimepata vyandarua? jeh! vinatundikwa? na vinatundikwaje?

"Kulala kwenye chandarua hiki kila siku kutakukinga dhidi ya maambukizi ya malaria" Fid Q akimsaidia kutundika mama wa kaya hii mwalimu Pendo Musa wa shule ya msingi Gedeli B.

Kwa mujibu wa Distinct coach bwana Timoth Lugejuna: Mtaa wa Nyakato mashariki jumla ya nyumba zipatazo 270 zimekaguliwa mpaka sasa ikiwa malengo ni kukagua nyumba 420. Twawashukuru sana na twawatakia usingizi mnono kwenye vyandarua vyenu pindi usiku utakapoingia. by ZINDUKA

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.