ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Monday, April 11, 2011

BINGWA NI YANGA AFRIKA -SIMBA MAHESABU YAWAONA 4-1< 3+deni 1. (<=ndogo kuliko)

Kiungo wa Yanga, Nurdin Bakari aliyetupia bao la kisigino lililotosha kufuta ndoto ya Simba ya kutetea ubingwa wake pamoja na timu hiyo ya mtaa wa msimbazi kupata karamu ya mabao 4-1 dhidi ya Majimaji.Mkuu wa mkoa wa Mwanza Abbas Kandoro akimkabidhi kombe la ubingwa Tanzania bara nahodha wa Yanga Shadrack Nsajigwa.

Kikosi kazi Yanga Afrika kilichoifunga Toto 3-0.

Abbas Kandoro akisalimiana na Kipa wa Yanga, Yaw Berko ambaye kama kawaida yake alitumia mbinu zote nyavu za goli lake zisitikisike kwani katika mchezo huo alipewa kadi ya njano dakika 22, baada ya kudaka mpira nje ya 18, baada ya kurudishiwa pasi fupi, lakini aliweza kuokoa faulo hiyo.

Kwa makiiini'' na nasaha za kuu wa mkoa wa Mwanza.

Hadi kipindi cha kwanza kinaisha hakuna aliyeweza kuchungulia goli la mwenzake lakini alikuwa kiungo Nurdin Bakari ndiye aliyeipatia Yanga bao la kuongoza dakika ya kwanza ya kipindi cha pili, kwa mpira wa adhabu nje ya eneo la 18, ile kuanza tu mchezo....'KITUuu!!' Nalo goli la pili likafungwa nae Davis mwape.

Nurdin akiwa amelipa mgongo goli alipokea mpira uliokuwa ukizagaa kwenye eneo la 18, kupiga kisigino na kumwacha kipa wa Toto Afrika, Hussein Tade aliyeingia kuchukua nafasi ya Wilbert Mwate akiruka uelekeo mwingine na mpira ukipenya kwa sataili ya aina yake hivyo kuipa Yanga bao la tatu.

Wachezaji wa Yanga mara baada ya goli la Nurdin Bakari (jezi no.5) wengine ni Jerry Tegete (10), Chacha Marwa (24) na Idd Mbaga (22). Kipa Tade aliingia uwanjani dakika ya 83 kuchukua nafasi ya Mweta aliyekuwa kikwazo kikubwa kwa Yanga, mara baada ya kupata maumivu ya paja.

Mabingwa hao wapya walianza mchezo huo taratibu na kuifanya Toto kutawala sehemu kubwa ya kipindi cha kwanza, lakini mambo yalibadilika nusu ya pili na kufanikiwa kupata mabao matatu muhimu.

Kombe la ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara lilipokuwa tayari kwa mabingwa wapya 2010-2011.

Yanga wakilionesha kombe lao kwa mashabiki waliofurika katika dimba la CCM Kirumba.

Tegete juu kwa juu na mashabiki wa Yanga, Timu hiyo imekuwa bingwa baada ya kufikisha pointi 49 sawa na timu ya Simba lakini imetawazwa bingwa baada ya kuwa na uwiano wa magoli 25 na 24 dhidi ya mahasimu wao Simba.

Mashabiki wa Yanga jijini Mwanza walifanya maandamano toka uwanja wa CCM Kirumba kupitia barabara ya makongoro hadi katikati ya jiji na hatimaye sikujuwa ila nauhakika ilikuwa either majumbani kwao ama sehemu za maraha kwani ilikuwa shangwe kwa ngoma, matrarumbeta na kupeperusha bendera.

ORODHA YA MABINGWA 2000-2011
2000 - Yanga
2001 - Simba
2002 - Simba
2003 - Simba
2004 - Simba
2005 - Yanga
2006 - Yanga
2007 - Simba
2008 - Yanga
2009 - Yanga
2010 - Simba
Na hatimaye ubingwa kwa mwaka..2011 = Yanga

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.