ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, March 25, 2011

MKUTANO WA ELIMU YA URAIA KUPITIA VYOMBO VYA HABARI WAFANYIKA DAR ES SALAAM HII LEO NA KUJA NA MAAZIMIO MAPYA YA MSINGI.

Mkutano juu ya elimu ya uraia kupitia vyombo vya habari hususani Radio na Luninga za vijijini umefanyika leo katika ukumbi wa Hotel Blue Pearl, jengo la Ubungo Plaza jijini Dar es salaam na kuhudhuriwa na wadau wakutosha toka pande na pande hapa nchini.

Juma Nyumano wa Radio Maria/Jogoo toka Mtwara.

Mkutano huo umeazimia kuanzishwa kwa mtandao wa kupashana habari na wanajamii, pia mkutano Umeshauri kuwa wataalam wa sheria wahusishwe kutoa elimu kwa waandishi wa habari juu ya jinsi ya kuchambua mapungufu ya katiba katika mchakato uliopo sasa wa marekebisho ya katiba.

Rachel Mabihya Mwakilishi wasikilizaji toka Sengerema, Mwanza.

Kutokana na mvuto walio nao Wasanii watumike katika kutoa elimu kuhusu katiba, wanawake wajiendeleze kiuchumi, vilevile vipindi maalum vya masuala ya jinsia vianzishwe kwenye radio na tv za jamii.

Wawasilisha mada kutoka kushoto Rose Haji na Sebastian Sanga.

Inatajwa kuwa asilimia 1 ya wananchi wanatumia mtandao wa Internet, asilimia 5 television na kuna maeneo mengine magazeti yanachukuwa zaidi ya siku mbili kufikia wasomaji hivyo kuchelewesha upatikanaji wa taarifa na habari hali inayopelekea wananchi kuishi katika mazingira ya habari za uvumi.

Kamati ikijadili mara baada ya mkutano kumalizika.

Mmkutano huo ulihitimishwa kwa kuundwa kamati ya kufuatilia na kuhakikisha yanafanyiwa kazi mambo yaliyoibuka ndani ya mkutano huo.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.