ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, March 26, 2011

ALIYEKIRI KUUWA WATU SABA AUHUKUMIWA KIFO

Mwanaume mmoja nchini Japani aliyekiri kuwaua watu saba jijini Tokyo, mwaka 2008 kwa kuendesha gari kwa kasi kwenye mtaa wa watu wengi na baadaye kutumia kisu kikali kuwamaliza wengine amehukumiwa adhabu ya kifo.

Tomohiro Kato aliendesha gari kwa kasi katika eneo la watembea kwa miguu katika mji wa kibiashara wa Akihabara uliopo katikati ya jiji la Tokyo na kupoteza maisha ya watu watatu pale pale. Kisha akatoka garini akiwa na kisu kikali na kuanza kuwachoma watu ovyo na kuwauwa watu wengine wanne .Wakati wa kesi yake, Kato mwenye miaka 28 alisema kuwa alichukizwa na unyanyasaji uliokuwa ukifanywa kwenye mtandao lakini kilichofanya Mahakama Kuu ya wilaya ya Tokyo imuhukumu kifo ni matamshi yake kuwa “Yeye anahusika na alifanya kwa makusudi shambulizi hilo lililouwa watu.

Jaji Hiroaki Murayama alisema kuwa mtu huyo aliwashambulia kwa kisu mtu yoyote aliyemsogelea baada ya kuzungukwa na hivyo kuleta mazingira yaliyohatarisha maisha ya watu ambao hawana hatia.Alisema kuwa ni tendo la jinai lililo na ukatili mkubwa.
“Sina kingine cha kuchagua zaidi ya kumuhumu adhabu ya kifo” , alisema Murayama.


KWAHISANI YA MIRINDIMO.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.