ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, March 23, 2011

MAADHIMISHO WIKI YA MAJI KITAIFA MWANZA

MAKAMU wa Rais , Dk. Mohamed Ghalib Bilal, jana alimezindua mradi wa maji vijijini wenye thamani ya Sh. Bilioni 19 utakaowanufaisha wakazi wa vijiji 44 vilivyopo katika mikoa ya Mwanza na Mara .

Awali akizindua mradi wa maji vijijini ambao umefadhiliwa na Serikali ya Japan, katika kijiji cha Hungumalwa kilichopo katika wilaya ya Kwimba mkoani Mwanza, amesema wananchi watakaofaidika nao wautunze ili kuhakikisha unakuwa endelevu kwa ajili yao na vizazi vijavyo.

Mh.Bilal akipata maelezo ya nyenzo maalum ya kuchuja maji kwa gharama ndogo (Tulip Water Filter) toka kwa mtaalam wa USAID.

SIMBA PIPE LINE.
Serikali ya Japani imetoa Yen bilioni 1.022 sawa na Sh. Bilioni 19.012 za Kitanzania kwa ajili ya kufanikisha mradi huo wa maji vijijini,na utaongeza watumiaji wa maji safi na salama katika vijiji 44 vilivyopo katika mkoa wa Mwanza na Mara.

Kwa upande wake Waziri wa Maji, Profesa Mark Mwandosya amesema hadi mradi huo utakapokamilika jumla ya visima virefu 182 vinavyotumia pampu za mikono vitachimbwa, hadi sasa vimeshachimbwa visima 116, ambavyo vimeshakamilika.

Maswi Drilling co.ltd nao waliwakilisha vyema viwanjani hapo.

Nje ya banda hili "Za sahizi" Kisha akasepa....

Tanzania breweries ltd (TBL) katika maadhimisho haya wameziwezesha shule nyingi mkoani Mwanza kupata maji safi na salama kwa kuchimba visima na kutoa mashine mbalimbali kwaajili ya urahisishaji wa upatikanaji maji.

Anaitwa Victor Maleko, Blogger maarufu toka rock City, Hapa inasakwa engo.....

Samaki ndani ya maji katika siku ya maji kwenye banda la Uvuvi.

Maadhimisho ya 23 ya wiki ya maji yamehitimishwa jana katika uwanja wa Nyamagana jijini Mwanza ambapo Dk. Bilal ametoa vyeti na vikombe kwa washiriki na washindi mbalimbali waliokuwa na mabanda kwenye uwanja huo kutokana na ubora wa huduma wanazozitoa kwa jamii.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.