ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, February 3, 2011

GHASIA ZACHUKUWA SURA MPYA MISRI.

Wafuasi wa Rais wa Misri, Hosni Mubarak wamekabiliana na waandamanaji wanaomtaka kiongozi huyo aondoke madarakani katikati mwa mji wa Cairo.Maelfu ya wafuasi wa Bw Mubarak walimiminika kwenye eneo la Tahrir na kuondoa vizuizi vilivyokuwa vimewekwa na waandamanaji.

Pande hizo mbili zilirushiana maneno kabla ya kuanza kurushiana mawe. Kuna Taarifa ambazo hazijathibitishwa zinasema maafisa wa polisi waliokuwa wamevalia kiraia walikuwa miongoni mwa baadhi ya wafuasi wa Bw Mubarak waliojitokeza katika eneo la Tahrir.

Athari za vurugu hizo.

Waandamanaji wanataka Rais Hosni Mubarak aondoke madarakani baada ya kutawala kwa muda wa miaka 30.

Mjini Cairo kwenyewe helikopta za kijeshi zimeendelea kuzunguka angani karibu na bustani ambapo maelfu ya watu walikusanyika licha ya amri ya kutotoka nje usiku iliyotangazwa na serikali.

Polisi waliagizwa kurejea kwenye barabara za mji wa Cairo walizoziacha siku ya Ijumaa, wakati yalipofanyika mandamanao makubwa ya kuipinga serikali. Mapambano mengine yameripotiwa kwenye mji wa Alexandria.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.