ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, February 4, 2011

MAJONZI YATAWALA MSIBA WA MAMA MZAZI WA MCHEZAJI WA ZAMANI WA TIMU YA PAMBA NA TAIFA STARS (FUMO FELICIAN).

Marehemu mama Teresa Felician Minde (1943-2011) aliyeaga dunia tarehe 1/2/2011.

Mume wa marehemu mzee Felician akitoa heshima zake za mwisho kwa mwili wa marehemu mkewe.

Huzuni ilitawala ilipofika zamu ya Watoto wa marehemu kutoa heshima zao za mwisho.

Diwani wa kata ya Nyamagana mh. Kotecha akiwafariji wafiwa.

Watoto wa marehemu katika picha hii ni mchezaji wa zamani wa timu ya Pamba ya Mwanza, Fumo Felician (kulia)na kaka yake Felix Felician anayefuata.

Fumo alizimia wakati akitoa heshima za mwisho kwa marehemu mama yake. Pichani akipata msaada toka kamati husika.

Sehemu ya wanandugu.

Jana jioni mara baada ya heshima za mwisho kutolewa mwili wa marehemu ulisafirishwa kwenda Bukoba mkoani Kagera kwaajili ya mazishi yanayotaraji kufanyika siku ya jumapili tarehe 6.feb.2011.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.