ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, February 17, 2011

7,7,3 WAVAMIA SOKO LA SAMAKI LA ILOGANZALA .

Jana wadau wa Leo tena, Kwa raha zetu na Club 10 walipata fursa ya kutembelea soko maarufu la samaki Iloganzala lililopo wilayani Ilemela jijini Mwanza na kujionea shughuli mbalimbali za biashara hiyo muhimu kwa uchumi wa watu waishio mkoani hapa.Wajaluo wanakauli 'Kamongo tamu sinda nyama' Chunguza mjomba utabaini!

Wadau wa Clouds jicho kwa jicho na matayarisho ya kamongo.

Ikiwa ni ahadi ya leo tena kukutana na BACHELA WA MWANZA kumpikia na kumpa 'full sevisi' za jikoni na haya ndo maandalizi yenyewe! Dina akinunua mboga MABACHELA MUPOOooooo!!

Gea Habib akitoa zawadi ya pasi kutoka ZEC.

Gea akitoa zawadi toka wadau wa Vifaa vya umeme ZEC ambao ni moja ya wadhamini wa 7,7,3 Mwanza.(miaka 7leo tena, 7kwaraha zetu na 3club kumi).

Wachuuzi wa samaki aina ya nembe.

Zamaradi akilisha ndege mwarabu wake.

Wapara samaki si kuparua magamba pekee hata kukutayarishia minofu, kinachobaki baada ya minofu kutolewa ndiyo chaitwa MAPANKI.

Dereva namba moja wa safari za 7,7,3 Mwanza, Paul Stone akiwa amebeba samaki aina ya kamongo.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.