ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, August 28, 2010

NI UNYAMA GANI HUU?!! AKATWA MKONO NA MUMEWE KISA SHILINGI ELFU 40.

MAMA CELINA VUNA MABOKO ANAYEISHI KIBONDO KIJIJI CHA LUGUNGA LUTALE MKOANI KIGOMA, AMENUSURIKA KIFO BAADA YA KUSHAMBULIWA KWA MAPANGA NA MUMEWE BW. MZONGOLI MABONDO (50) TUKIO HILO LILITOKEA WIKI MOJA ILIYOPITA NYUMBANI KWAKE HUKO KTK KIJIJI CHA LUTALE.

MAJEREHA YA KICHWANI.

KATIKA TUKIO HILO MAMA HUYO LICHA YA KUPATA MAJERAHA MABAYA KICHWANI, ENEO KUBWA LA MGONGONI NA SEHEMU ZA BEGA LA KUSHOTO VILEVILE MWANAMAMA CELINA KAKATWA KABISA MKONO WAKE WA KUSHOTO NA KUBAKIA KIGUTU'.

SABABU ZA KUTOKEA KWA TUKIO HILO LA KIKATILI NI MUME KUDAI MAMA HUYO AMRUDISHIE PESA ZAKE SHILINGI ELFU 40 ALIZOTOZWA KWENYE OFISI YA MTENDAJI WA KIJIJI KUMLIPA FIDIA MAMA CELINA BAADA YA MUME HUYO KUZICHOMA MOTO NGUO (KANGA, VITENGE NA BLAUZI)ZA MKE HUYO WA KWANZA KISA AKIMTUHUMU MAMA HUYO KULA MAHALI ISIYOFAHAMIKA YA BINTI YAO WA KWANZA.

MAJIRA YA SAA 3 MARA BAADA YA CHAKULA CHA USIKU CELINA AKIWA NA MWANAE MDOGO JESKA WALISIKIA MLANGO UKIGONGWA KWA NGUVU NA MUMEWE HUYO BW. NZONGILI MABONDO.
NDIPO MLANGO UKAFUNGULIWA NA MTOTO JESCAR.
MKONONI AKIWA AMESHIKA PANGA BW. NZOGOLI AKAINGIA KWA GHADHABU NDANI YA NYUMBA HIYO NA KUANZA KUMJERUHI KWA PANGA MKEWE CELINA HUKU AKIMKARIPIA "UTANILIPA PESA YANGU ELFU AROBAINI..." MAPANGA YAKAENDELEA TWAAA!, SHWAAA!, PAAA! MWISHOWE MUME HUYO KUONA AKIELEWEKI AKATIMUA NA MKEWE WA PILI ALIYE SINDIKIZANA NAE HADI NYUMBA YA BI MKUBWA KISHA KUACHWA CHINI YA MTI NJE, WAKATI BWANA HUYO AKIFANYA UNYAMA HUO.

DAKIKA CHACHE BAADAE MAJIRANI WAKAFIKA ENEO LA TUKIO NA KUFUATIWA NA POLISI, NDANI YA NYUMBA WAKIKUTA DAMU ZIKIWA ZIMETAPAKAA NAE MAMA CELINA AKIWA HAJITAMBUI, NDIPO WALIPOCHUKUWA JUKUMU LA KUMKIMBIZA KWA AMBULANCE HADI HOSPITALI YA BUGANDO JIJINI MWANZA.

CELINA AMBAYE KWA HIVI SASA ANAENDELEA KUPATA MATIBABU BUGANDO HOSP ANASEMA ALISHITUKIA YUKO KWENYE KITANDA ASIJUWE WAPI, AKIWA AMEZUNGUKWA NA MADAKTARI. NA ANASEMA ALILIA SANA SIKU YA PILI POLISI WALIPOMLETEA KIPANDE CHA MKONO WAKE WA KUSHOTO KILICHOKATWA AMBACHO HAKIKUWEZA KUUNGIKA TENA. INGAWA HANA MSAADA KWA SABABU NDUGU ZAKE NA MARAFIKI WAKO MBALI, LAKINI HALI YA MAMA HUYO INAENDELEA VIZURI.

MTUHUMIWA AMETOWEKA NA ANASAKWA NA JESHI LA POLISI, NAYE MKE MDOGO YUKO MAHABUSU.

HIMA KWA YEYOTE MWENYE MSAADA.

HAPBORZDEI ANKAL!!!!

YULE MBLOGISHAJI MAARUFU NCHINI (LONG TIME KWENYE GAME) ISSA MICHUZI -EI KEI EI- 'ANKAL' LEO NI SIKU YAKE YA KUZALIWA.
Ankal (KULIA) akipongezwa na mgombea ubunge wa Kasulu Mashariki Bw. Jamal Abdallah walipokutana usiku wa kuamkia leo mjini Kigoma. Bw. Abdallah, ambaye ni mdogo wake mchambuzi wa kandanda Dokta Liky Abdallah, alishinda kwa kishindo katika kura za maoni na kumwondoa aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo Bw. Kilontsi Mpologomyi na wagombea wengine.

MNOMBA NJAIDI AFARIKI DUNIA.

SOGGY, TIRA HASSAN NA MAREHEMU MNOMBA ENZI ZA UHAI WAKE.

MNOMBA NJAIDI AMBAYE ZAMANI ALIKUWA MENEJA WA KITUO CHA REDIO TRIPLE A YA MJINI ARUSHA AKISHIRIKI KAMA DJ NA PROMOTER, AMEAGA DUNIA JANA USIKU MJINI CORK, NCHINI IRELAND. INAELEZWA KUWA MAREHEMU ALIPATA STROKE MAJIRA YA USIKU HATA MAUTI KUMKUTA.

Mungu ailaze roho ya marehemu mahala pema peponi
Amin.


HABARI PICHA KWA HISANI YA MICHUZI JR.

Friday, August 27, 2010

KENYA YAONGOZWA KWA KATIBA MPYA.

MWAI KIBAKI AKITIA SAINI.

Kenya imeandika historia mpya ya utawala nchini humo kwa kuidhinisha katiba mpya, iliyotungwa na wananchi wenyewe, baada ya ile iliyokuwa ikiitumia kabla ya kupata uhuru wake mwaka 1963.

Rais Mwai Kibaki, aliwaongoza maelefu ya raia wake walioshuhudia akitia saini katiba mpya ya nchi hiyo katika sherehe zilizofanyika viwanja vya Bustani ya Uhuru mjini Nairobi siku ya Ijumaa.

Baada ya kutia saini nakala sita za katiba hiyo, wimbo wa taifa la Kenya ukapigwa na kufuatiwa na mizinga 21 ya heshima.

Rais Kibaki, Waziri Mkuu Raila Odinga, Makamu wa Rais Kalonzo Musyoka, Spika wa bunge na wabunge wamekula kiapo cha kuilinda, kuitetea, na kuiheshimu katiba hiyo mpya kwa manufaa na ustawi wa taifa la Kenya na watu wake.

MWELEKEO MPYA.
Katiba hiyo imepangwa kuzuia aina yoyote ya vurugu kama zile zilizofuatia baada ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2007, wakati zaidi ya watu elfu moja waliuawa kutokana na mgogoro wa kupinga matokeo yaliyompa ushindi Rais Kibaki.

Pia ina udhibiti mkubwa kuhusu madaraka ya rais, na inatoa madaraka kwa serikali za majimbo na kuwaongezea uhuru wananchi.


UTATA.
Miongoni mwa viongozi wa mataifa ya kigeni waliohudhuria ni Rais Omar Al Bashir wa nchi jirani ya Sudan ambaye anatakiwa na mahakama ya kimataifa inayoshughulikia uhalifu wa kivita, kwa tuhuma za kuendesha mauaji ya halaiki katika jimbo la Darfur nchini Sudan.

Kufika kwake katika sherehe hizo kumeonekana kuyakera baadhi ya makundi yakiwemo ya haki za binadamu na mabalozi hususan kutoka nchi za magharibi.

Afisa mkuu wa Tume ya Kutetea Haki za Binadamu nchini Kenya, Muthoni Wanyeki ni miongoni mwa watu walioishutumu serikali ya Rais Kibaki kumwaalika kiongozi huyo wa Sudan.

Wanyeki amekaririwa akisema " Ni aibu kwa Wakenya ambao waliuchagua utawala ambao unatakiwa kusimamia hazi za binadamu na badala yake wamekiuka hilo, jambo ambalo dhahiri linaashiria mwisho wa kuwaadhibu wakosaji si tu nchini Kenya bali katika ukanda huu wa Afrika.

Amesema, "Si mwanzo mwema wa utekelezaji wa katiba mpya. Katiba Mpya inabainisha wazi kuwa tunawajibika kutekeleza mikataba yote ya kimataifa ambayo tumeridhia, ikimaanisha tunalazimika kushirikiana na mahakama hiyo ya ICC."

Hata hivyo, serikali ya Kenya imetetea uamuzi wake wa kumwalika Rais Omar al Bashir, kuhudhuria sherehe hizo.

Akizungumzia wito wa kuitaka Kenya kumkamata Rais huyo wa Sudan, Waziri wa mambo ya nje wa Kenya, Moses Wetangula, amekaririwa akisema, Rais Bashir yupo nchini hapa kwa mwaliko uliofanywa na serikali ya Kenya kwa jirani zake wote kuwaomba kuhudhuria tukio hili la kihistoria.

Bw Wetangula amesema, "Kenya haijavunja sheria yoyote na ni nchi huru, hivyo ina haki ya kumwalika yeyote inayetaka aje hapa nchini."

Kuhusu kutomkamata Rais Bashir kama ambavyo nchi wanachama wa mahakama ya ICC wanatakiwa kutekeleza agizo la mahakama hiyo, Wetangula amesema, "Huwezi kumdhuru au kumfedhehesha mgeni wako, huu si utaratibu, desturi na maadili ya Kiafrika."


KWA HISANI YA BBC SWAHILI.

'WANA HIP HOP' FID Q NA BABA LUKU NDANI! TAREHE 18 SEPT 2010 TUNZA LODGE PATAKUWA HAPATOSHI! BURUDANI NA SANAA KUTAWALA .

ZAIDI ya watoto 50 wanaoishi katika mazingira magumu na wale wanaolelewa katika vituo vya watoto yatima kutoka katika mikoa ya Arusha,Dar es Salaam pamoja na Mwanza wanatarajia kushirika maonyesho ya Earthdance jijini hapa.

BANGO LA KUELEKEZA TUNZA LODGE.

Maonyesho yatafanyika katika nchi 80 maeneo 500 ya nchi hizo ambapo Tanzania itakuwa inashiriki kwa mara ya kwanza katika kufanya maonyesho hayo ambayo huwa yanafanyika kila mwaka Septemba 18.

UFUKWE TULIVU WA TUNZA LODGE.

Mratibu wa maonyesho hayo Ben Mwangi amesema kuwa siku hiyo maalum watu hukusanyika ktk sehemu mbalimbali duniani na kufanya maombi ya amani. Maombi hayo huwa yanaambatana na muziki wa dansi wa asili ambao huwa unalenga kudumisha mila na destuli za makabila husika.

UFUKWE WA ZIWA VICTORIA MAJI BARIDI.

Wasanii wakali wa hip hop kama Fid Q toka TZ na Baba luku toka UGANDA kupamba stage la burudani.Asilimia 50 ya fedha ambazo watazipata katika maonysho hayo kutoka katika kingilio zitaenda kwa watoto yatima wa kituo cha kuleana jijini Mwanza ambapo zitatumika kuwaendeleza katika miradi yao.

TUNZA LODGE KWA NJE.

Wanachi watao udhuria maonyesho hayo watapata fursa ya kuona maonyesho ya mavazi ya kimasai pamoja na kupata fursa ya kupiga picha wakiwa katika mamevaa mavazi hayo ya asili.



NGOMA YA WASUKUMA.

Maonyesho hayo yamedhaminiwa na kampuni ya bia TBL kwa kupitia bia ya Kilimanjaro ambapo zawadi mbalimbali na michezo kuwepo SIKU HIYO.

HAPPY BIRTHDAY BROTHER.

ESTER KHERI KUTOKA MUSOMA MKOANI MARA KANITUMIA PICHA NA ANAZUNGUMZA HIVI JUU YA MY HAZBAND WAKE..
"mambo vp mr uwiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii! upo poa naomba nikutumie picha kwa ajili ya bithrday ya ma husband. Anaitwa Kheri Mchume aka baba Mariam"

BLOGU HII INAKUTAKIA KILA LA KHERI KATIKA MAISHA YAKO ENDELEA KUITEKETEZA MISHUMAA KAMANDA.

Wednesday, August 25, 2010

NIMESOMA BANGO PALE ABIRIA CHUNGA MZIGO WAKO' MIE NAUCHAPA USINGIZI SAFARINI!


KATIKA SAFARI YANGU ILIYOANZA YA SAA 12 ASUBUHI HADI SAA 2 USIKU ILITAWALIWA NA USINGIZI HASA NYAKATI ZA MCHANA.

TAMAA YANGU KUBWA ILIKUWA KUPATA PICHA ZA VIJIJI NA MAISHA YA WATANZANIA MKOA KWA MKOA, TATIZO SASA NILIKUWA NASINZIA ILE KINYAMA' NA KILA NIKIZINDUKA BABAKE! NAONA PORI NA MASHAMBA, KWAMBA SEHEMU ZA MIJI TAYARI TUMEZIPITA. 'KUNDA-NDA-NDEKI'

LAKINI NAPATA VITU DIFERENTI' SAFARINI.

MWISHO WA SIKU NIKAWA NAZIJADILI SASA.. PICHA NILIZOPIGA NJIANI NINI KIMESABABISHA KUTOTIMIZA LENGO. jibu likawa: USINGIZI.


KWA KAWAIDA USINGIZI UNACHUKUWA THELUTHI MOJA YA MUDA WA MAISHA YOTE KWA BINADAMU, NA UNAHUSIANA KWA KARIBU NA AFYA YA WATU. USINGIZI BORA NA WAKUTOSHA NI MSINGI MUHIMU WA AFYA. LAKINI WATU WENGI HATUFAHAMU SAYANSI YA USINGIZI KWAMBA BINADAMU ANAHITAJI USINGIZI KWA SAA NGAPI? NI KWA VIPI ANAWEZA KUUBORESHA USINGIZI? INAFAA KULALA MCHANA AU?


JE NI VYEMA KULALA SAFARINI? BILA SHAKA JIBU NI SI VYEMA KWANI VYOMBO VYA USAFIRI VINA TAHADHARI ZAKE, NA NI RAHISI KWA MSAFIRI KUPATA TAARIFA YA TAHADHARI IKIWA ATAKUWA MACHO.

'ABIRIA CHUNGA MZIGO WAKO' HIVYO MSAFIRI NI KAMA MLINZI WA DORIA. KULALA KOSA LA JINAI.

KUHUSU KULALA MCHANA AU ADHUHURI: WATAALAM WANASEMA USILALE KWA MUDA MREFU SANA MAJIRA HAYO, DAKIKA 10 HADI NUSU SAA INATOSHA. KWA SABABU UKILALA KWA MUDA MREFU NA KUINGIA KWENYE USINGIZI MZITO, ITACHUKUWA MUDA KURUDISHA UFAHAMU WA KAWAIDA KUTOKA USINGIZINI KWA KUWA UFAHAMU HUTOWEKA KIKAMILIFU WAKATI WA USINGIZI MZITO.

UMEJIFUNZA JAMBOeeeee!!!!! SEMA NDIYO NDIYO!!

Tuesday, August 24, 2010

TIGER WOODS NA MKEWE WATALIKIANA.

BINGWA WA MCHEZO WA GOLF DUNIANI TIGER WOODS AMETALIKIANA NA MKEWE ELIN NORDEGREN. HIZI NI HABARI KUTOKA MTANDAO WA MCHEZAJI GOLF NAMBA MOJA DUNIANI.

KWA PAMOJA WALISEMA "Tunasikitika kuwa ndoa yetu imefikia tamati na tunatakiana kila la heri katika mustakabala wetu," WAWILI HAO WALISEMA.


HATA HIVYO WAWILI HAO WAMESEMA WATASAIDIANA MAJUKUMU YA KULEA WATOTO WAO WAWILI. SUALA LA KUGAWANA PESA HALIJAWEKWA WAZI LAKINI TAARIFA KATIKA VYOMBO VYA HABARI VYA MAREKANI ZINASEMA KUWA BI.NORDEGREN HUENDA AKAONDOKA NA KITITA CHA DOLA MILIONI 100.

WOODS AMEKUWA NA MATATIZO KWENYE NDOA YAKE HALI ILIYOMPELEKEA KITETE HATA KUPATA AJALI PINDI SAKATA LIKIELEKEA KUNUKA, BAADAE MZEE MZIMA MZIGO UKAMWELEMEA AKAOMBA SAMAHANI HADHARANI HUKU AKIKIRI WAZI KUWA NA UHUSIANO WA KIMAPENZI NA WANAWAKE KADHAA NJE YA NDOA.

NAAM HAYO NI YA WOODS NA MTALAKA WAKE, KILA LA KHERI KATIKA MAISHA YAO MAPYA KILA MTU KIVYAKEzzz!

!!!NYABULEBHEKA HILI HAPA!!!

MWONEKANO KWA PICHA YA KAWAIDA.



MWONEKANO KWA PICHA YA VIDEO.

KWA MARAFIKI AMBAO TULOKUWA TUKISUMBUANA JIWE - JIWE!

HAYA SASA LILE JIWE LINALOCHEZA (NYABULEBHEKA) HILI HAPA INGAWA SIKULINASA VIZURI KWA KIKAMERA CHANGU KIDOGO UKIJUMLISHA NA KUTETEMA KAZI KWELI KWELI!!

Monday, August 23, 2010

MAVITUzz!! DUNIANI YANAENDELEA YA KIPEKee! MVUTO BILA KOROMBWee! WACHA NIKUSOGEZee!

CHAMA LA MWANANGU MWENYEWE, TEMBELEA KISHA UNAMBIEeee!

HATIMAYE TIBA YA EBOLA YAPATIKANA.


Serikali nchini Marekani imetoa ruhusa kwa majaribio kufanyika kwa wanaadamu baada ya dawa hiyo kugundulika kuwa tiba kwa tumbili. Ebola ni moja ya maradhi mabaya na yanaua.


Ugonjwa wa Ebola ni hatari zaidi kwa tumbili kuliko binaadamu.Wakipatikana na ugonjwa huu wanafariki dunia.

Lakini kwa majaribio ya dawa hii,asilimia sitini walitibiwa.Matumaini ni kwamba matokeo haya mazuri yatajitokeza au yawe bora zaidi wakati dawa hii itakapotumiwa kwa binaadamu.

Ebola imeua takriban watu elfu moja mia mbili tangu ilipogunduliwa katika miaka ya sabini nchini Zaire,sasa Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo. Mara nyingi mlipuko wa ebola hutokea barani Afrika.



MADAKTARI NDANI YA MAABARA.

Ebola inaweza kuambukizwa kutokana na maji maji ya mwili. Dalili zake ni pamoja na kutapika huku walioathirika wakitoka damu pamoja na viungo muhimu vya mwili kushindwa kufanya kazi kabla hawajafariki dunia. Kutokana na kuwa na athari kubwa inahofiwa kuwa virusi vya ebola vinaweza kutumika kwa ugaidi.

Ufadhili wa utafiti ulitiliwa nguvu Marekani kufwatia mashambulio ya septemba kumi na moja mwaka 2001.

Dawa hii mpya imefanyiwa utafiti na idara ya utafiti ya jeshi la Marekani pamoja na kampuni nyengine binafsi ya AVI-BioPharma.


HABARI KWA HISANI YA BBC SWAHILI.

Sunday, August 22, 2010

JK NA KURA ZAKE ZA 'NDIYO' JIONI YA LEO MKOANI MWANZA.

WAGOMBEA MADIWANI.

WANAFUNZI TOKA VYUO MBALIMBALI WALIOSHIRIKI KUSHOW LOVE KWA MGOMBEA WAO KITI CHA URAIS DR.JAKAYA.

MARLOW AKITIKISA KTK BURUDANI.

SEHEMU YA NYOMI LA WAUNGWANA WA MWANZA WALIOJITOKEZA KUSIKILIZA SERA ZA CCM.

WASANII WALIOSHEREHESHA UMMA ULIOFIKA UWANJA WA CCM KIRUMBA MZ KTK PICHA YA PAMOJA BAADA YA KUPEANA MKONO NA JK AMBAYE ALITOBOA SIRI YAKE YA MOYONI KUWA YEYE YU MPENZI SANA WA MUZIKI WA BONGO FLEVA, INGAWA HACHEZI KWA MWILI BALI KWA KUTIKISA KICHWA KUTOKANA NA KASI YA MZIKI HUO. AMESISITIZA KUIENDELEZA SERA YAKE YA KUWASAIDIA WASANII FANI ZOTE.

FLORA MBASHA NA KUNDI LAKE SHUGHULINI.

DIAMOND ALING'AA KWELI KAMA JINA LAKE (ALMASI).

MARLOW NA KIDUKUZzz MKONONI VUVUZELA.

JUMA NATURE NA WANAUME HALISI NI BARRrra!!

WASOMI WALIOJITOKEZA KUSIKILIZA SERA.

MIE NA MWANANGU MWENYEWE NATURE.

MH. UNATISHA SERA ZIMEKUBALIKA!!!MGOMBEA UBUNGE JIMBO LA ILEMELA MH. DIALO AKIWA NA WADAU WA CCM. DUH ILIKUWA KAZI KWELI KWELI KWANI WATU WALIKUWA WAKING'ANG'ANIA KUPIGA NAE PICHA.

SPIKA WA ZAMANI MH.PIUS MSEKWA NA WANA CCM.

JK ALIPOWASILI AIR PORT MWANZA AKIPEANA MKONO NA MH. LAWRENCE MASHA AKIFUATIWA NA MH. WILLIAM NGELEJA KISHA MWISHONI NI BW. LAMECK AIRO MBUNGE MTARAJIWA ALIYEMWANGUSHA KWA KISHINDO KURA ZA MAONI PROF. FILEMON SARUNGI.

KAMWE USILETE MASHEUZI BARABARANI.

NAJUA WADAU MWASUBIRI KWA HAMU KUIONA VIDEO JAPO KIDUCHU YA JIWE LA NYABUREBHEKA (JIWE LINALOCHEZA) NAAHIDI SOON KULITUNDIKA.

LAKINI KWA LEO CHEKSHIA AJALI ILIYOMKUTA MSELA WANGU WAKATI AKIJISHAUWA BARABARANI.




KAMWE USIJARIBU!!