ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Tuesday, December 14, 2010

ASKARI MAGEREZA MWANZA AJILIPUA KWA RISASI.

Askari magereza mwenye namba B50004 Elias Bukwima amekufa kwa kujifyatua risasi tatu kichwani kwa kutumia bunduki aina ya smg yenye namba za usajili D61220 aliyokuwa akiitumia kazini.

Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo mapema leo kamanda wa polisi mkoa wa Mwanza Simon Sirro amesema kuwa tukio hilo lililotokea jana majira ya saa saba mchana wakati askari huyo akiwa eneo la lindo kwenye gereza la Butimba jijini Mwanza.

Maiti ya askari huyo imehifadhiwa katika hospitali ya Rufaa ya Bugando huku polisi wakiendelea kufanya uchunguzi kubaini chanzo cha mauaji hayo.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.