ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, December 18, 2010

ABOU SEMHANDO AFARIKI DUNIA KWA AJALI.

ENZI ZA UHAI WAKE ABOU SEMHANDO.
Taarifa zilizopatikana asubuhi hii na kuthibitishwa na mmoja wa mashuhuda wa tukio hilo zinamtaja mpiga drums maarufu nchini kutoka bendi ya African Stars wana wa kutwanga na kupepeta, Abou Semhando amefariki dunia usiku wa kuamkia leo maeneo ya Tangi bovu, Mbezi jijini Dar es salaam. Imeelezwa kuwa marehemu Abou Semhando alikuwa akiendesha pikipiki ghafla akakumbana na gari nalo likamgonga hivyo kufariki papo hapo.

PIKIPIKI ALIYOKUWA AKIENDESHA MAREHEMU ABOU SEMHANDO.

GARI LILILOMGONGA MAREHEMU NA MASHUHUDA WA AJALI HIYO WAKITATHMINI.
Kwa sasa msiba wa mwanamuziki huyo upo nyumbani kwake Mwananyamala.
Tutaendelea kupeana taarifa zaidi...

PICHA NA HABARI KWA HISANI YA MICHUZI JR.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.