ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Tuesday, November 30, 2010

BEI MPYA YA SODA ZA COCA COLA KANDA YA ZIWA YATAMBULISHWA SAMBAMBA NA MOTISHA.

Kampuni ya Coca cola Nyanza Bottling company limited (NBCL) leo imetangaza rasmi bei mpya za soda zake, akitangaza bei hizo Mkuu wa mauzo na masoko wa kampuni hiyo bw. Bhubhinder Singh amezitaja bei hizo ni kama ifuatavyo...
Bei ya soda za kampuni hiyo zimepanda kutoka shilingi 400 kwa ujazo wa chupa ya ml350 hadi shilingi 500 kwa ujazo huo huo. Coca cola inawasihi wateja wake wote kutolipa zaidi ya shilingi 500 katika ununuzi wa soda kama ilivyoainishwa kwenye jedwali hapo juu.
Bei hiyo halali itatambulishwa kwa nguvu zote kupitia vyombo mbalimbali vya habari, mabango, vipeperushi kwenye sehemu za mauzo, kwenye friji za mauzo, kalenda zitakazotoka za mwaka 2011, t-shirts, kofia na promosheni za mitaani ili kutusaidia hata pale tunapokwenda sehemu za vijijini tusibamizwe na wauzaji, kwani kwa vijijini bei ni hiyo ya 500 hata kabla haijapanda kihalali.
Bei ya kreti moja inapanda kutoka 8,100 hadi 9,600 huku faida ya muuzaji ikipanda kutoka asilimia 18 na kuwa asilimia 25.
Kampuni hiyo imetoa changamoto kwa wadau wake kwa kuwazawadia chupa 3 za vinywaji bure kwa kila kreti moja watakalonunua kuanzia tarehe 1 hadi 10 december 2010 na kuanzia december 11 hadi 20.2010 Nunua kreti moja upate chupa mbili za vinywaji.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.