ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Tuesday, July 13, 2010

UKANDA MAALUM WA BOMU WAKUTWA UGANDA.

Maafisa wa Uganda wamesema, ukanda unaotumiwa na walipuaji mabomu wa kujitoa mhanga ambao haujalipuka umepatikana mjini Kampala baada ya shambulio la Jumapili lililotokea kwa watu waliokuwa wakitazama fainali ya Kombe la Dunia kupitia televisheni.

Wamesema kuna watu ambao idadi yao haijajulikana wamekamatwa.

Takriban watu 74 waliuawa katika milipuko miwili iliyotokea katika klabu ya raga na kwenye mgahawa.

Kundi la wapiganaji la Kisomali la al-Shabab limesema linahusika na mashambulio hayo kwasababu Uganda inaiunga mkono serikali ya Somalia mjini Mogadishu.


Msemaji wa serikali Fred Opolot amesema ukamataji ulifanyika baada ya ukanda huo kukutwa katika eneo la Makindye kusini mashariki mwa Kampala.

Polisi wamesema, ukanda huo ulikutwa kwenye mfuko mweusi kama ule unaotumika kubebea lap-top kwenye klabu ya usiku Jumatatu mchana.

Mfuko huo ulikuwa na milipuko na mabomu.

Mataifa ya watu hao waliokamatwa hayajatajwa lakini maafisa wamesema kichwa kimoja kilichopatikana karibu na eneo moja lilipotokea mlipuko huo kinaonekana kuwa cha Msomali, ambaye huenda alikuwa amejitoa mhanga.

CHANZO CHA HABARI BBC SWAHILI.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.