ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Monday, March 18, 2024

MWENYEKITI WA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA MIUNDOMBINU AWATAKA WAKALA WA MAJENGO KUFANYA HAYA.

 NA ALBERT GSENGO/MWANZA

Mwenyekiti wa kamati ya kudumu ya Bunge ya Miundombinu Seleman Kakoso amewataka wakala wa Majengo Tanzania TBA kuwa na ubunifu katika ujenzi wa majengo mazuri na yenye mvuto wa kibiashara ili wawe na uwezo mkubwa wa kukusanya kipato chao binafsi na kuacha kuitegemea serikali. Kakoso amesema hayo alipotembelea na kukagua mradi wa ujenzi wa jengo la kupangisha lililopo eneo la Ghana wilayani Ilemela jijini Mwanza na kuongeza kwa kumwagiza waziri wa ujenzi Innocent Bashungwa kuhakikisha anawasaidia TBA waweze kukusanya madeni ambayo wanaidai serikali kupitia taaisisi zake. Kwa upande wake Mtendaji Mkuu wa TBA Daud Kondoro amesema ujenzi wa jengo hilo umefikia asilimia 50 ambapo amesema wao kama TBA waliona Jiji la mwanza lina uhitajia mkubwa wa Majengo ya kupangisha hivyo ni wajibu wao kuyaendeleza maeneo yote nchi nzima. #samiasuluhuhassan #jembefm #mwanza

MAKARANI WA KUSIMAMIA UCHAGUZI UDIWANI KATA YA MSANGANI WAPIGWA MSASA


 NA VICTOR MASANGU KIBAHA


Katika kuelekea katika uchaguzi mdogo wa kujaza nafasi ya Udiwani kata ya Msangani iliyopo Halmashauri ya mji Kibaha makarani wa kusimamia uchaguzi huo wamepatiwa mafunzo maalumu kwa mujibu wa sheria na taratibu zilizowekwa.

Uchaguzi huo wa kujaza nafasi ya udiwani wa kujaza  nafasi hiyo unnatarajiwa kifanyika machi 20 mwaka huu ambapo utawashirikisha wananchi wa kata ya Msangani.

Kadhalika  Makarani hao  waongozaji licha ya kupata  mafunzo hayo wamepata  kiapo cha kutunza Siri Chini ya Kanuni ya 16(1) (a) na 50 (4) ya Kanuni za Uchaguzi wa Rais na Wabunge,2020 na Kanuni ya 14 (1)(a),(2) na 43(4) ya Kanuni za Uchaguzi wa Serikali za Mitaa (Uchaguzi wa Madiwani),2020 Mbele ya Msimamizi wa Uchaguzi Salum Papen.

Aidha,Mafunzo hayo yametolewa na Maria Israel,Benjamin Mputtu wakisaidiana na Afisa Uchaguzi wa Halmashauri ya Mji Kibaha Optuna Kasanda ambao wamewasisitiza kwenda kufanyakazi kwa kuzingatia Sheria,Kanuni na taratibu za Uchaguzi

Akifungua Mafunzo hayo,Msimamizi wa Uchaguzi,Mwanasheria nguli wa Mahakama kuu na zilizo chini yake Salum Papen amesema.." _Tume imewateua ninyi kwa mujibu wa sheria na Kwa kuzingatia uzoefu wenu katika masuala ya Uchaguzi_ "katendeni haki amesisitiza Papen

Papen ametoa rai kwa Makarani waongozaji kujiamini na kujitambua,kufanyakazi kwa kuzingatia Katiba ya Nchi,Sheria za Uchaguzi na Kanuni zake,Maadili ya Uchaguzi na Maelekezo mbambali yanayotolewa na Time

Katika hatua nyingine Makarani wametia tamko la kujitoa uanachama au kutokuwa na Chama cha Siasa chini ya Kanuni ya 16 (1)(b) na ( 3 ) ya Kanuni za Uchaguzi wa Rais na Wabunge,2020 na Kanuni 14(1) (b) na (3) ya Kanuni za Uchaguzi wa Serikali za Mitaa,(Uchaguzi wa Madiwani),2020 mbele ya Msimamizi wa Uchaguzi,Mwanasheria Salum Papen

Aidha,Andrea Isamaki Ofisa kutoka Tume ya Taifa ya  Uchaguzi (NEC) ameshiriki kushuhudia Mafunzo,kiapo cha kutunza Siri na tamko la kujitoa uanachama kwa Makarani waongozaji

Nadia Issa na Benson Shawa,Makarani waongozaji wamesema wanakwenda kufanya kazi kwa weledi mkubwa kwa kuzingatia Sheria,Kanuni na taratibu za Uchaguzi 

Uchaguzi mdogo wa kujaza nafasi ya udiwani katika Kata ya Msangani unatarajiwa kufanyika machi 20 mwaka huu  kutokana na kifo cha Mhe.Leonard Mlowe kilichotokea tarehe 23 Disemba,2023 ambapo jumla ya vyama nane (8) vya Siasa vinatarajia kushiriki.

Saturday, March 16, 2024

LIVERPOOL WAPEWA ATALANTA ROBO FAINALI EUROPA

 

LIVERPOOL itacheza na Atalanta katika robo fainali ya Europa huku West Ham ikipangwa kumenyana na Bayer Leverkusen.

‘The Reds’ ambao wapo kwenye mashindano ya EPL, Europa, FA bado wana uwezo wa kutwaa mataji   katika msimu wa mwisho wa Jurgen Klopp.

Wapinzani wa Italia, AC Milan na Roma wanakutana kugombea nusu fainali, huku klabu ya Benfica ya Ureno ikimenyana na Marseille ya Ligue 1.

Raundi ya kwanza itafanyika Aprili, 11 na Aprili 18 raundi ya pili.

TEMESA YAANZA KUFANYIA KAZI MALALAMIKO YA WATEJA

 

SIMIYU: Wakala Wa Ufundi na Umeme (TEMESA) imeanza kufanyia kazi malalamiko ya wateja wake, ambao wengi walilalamikia gharama kubwa za matengenezo ya magari, pamoja na matengenezo yasiyofikia viwango.

Malalamiko mengine yalikuwa ucheleweshaji wa matengenezo, uwepo wa mafundi wasiokuwa na uwezo, na uadilifu, uhaba wa vipuli, pamoja na kutokuwa na vitendea kazi vya kutosha.

Hayo yamesema leo na Mkurugenzi wa Huduma za Ufundi (TEMESA), Hassan Karonda alipomwakilisha Mtendaji Mkuu wa taasisi hiyo wakati wa kikao cha wadau wa TEMESA Mkoa wa Simiyu.

Karonda amesema kuwa changamoto ya gharama za matengenezo, TEMESA imeingia mkataba na wazabuni zaidi ya 56 kwa ajili ya kutoa huduma ya vipuli pamoja na vilainishi kwa gharama nafuu.

“ Gharama kubwa ambazo wateja wetu walikuwa wanalalamikia asilimia 70 zilitokana na vipuri na vilainishi, katika mkakati wetu mpya tumeingia mkataba na wazalishaji moja kwa moja wa bidhaa hizo ambazo wanatupatia kwa gharama nafuu,” alisema Karonda.

Kuhusu mafundi wasiokuwa na ujuzi, weledi na uadilifu, Mkurugenzi huyo alisema kuwa wameingia mkataba na Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya ufundi stadi (VETA) kwa ajili ya kuwapatia mafundi wenye ubora ujuzi wa kutosha.

“ Karakana zetu zote nchi nzima tumefunga kamera ili kukomesha wafanyakazi wasiokuwa na weledi na uadilifu na mpaka sasa zaidi ya watumishi 7 wakiwemo mafundi wamechukulia hatua za kisheria ikiwemo kufukuzwa kazi katika mikoa ya Dodoma na Kigoma,” alieleza Karonda.

Alisema kuwa mbali na hilo Serikali ya Rais Samia Suluhu Hassan kwa mwaka huu wa fedha imetoa kiasi cha Sh milioni 700 kwa ajili ya ununuzi wa vitendea kazi lengo likiwa kuboresha utendaji kazi wa taasisi hiyo.

Akifungua kikao hicho kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa, Mkuu wa Wilaya ya Itilima, Anna Gidalya alizitaka taasisi zinazodaiwa na TEMESA kuhakikisha zinalipa madeni yao ili taasisi hiyo iweze kutekeleza majukumu yake ipasavyo.

RC TANGA ATAKA UBUNIFU WAKUU WA WILAYA.

 

TANGA: Mkuu wa Mkoa wa Tanga Balozi, Batilda Burian amewaapisha wakuu wa Wilaya ya Pangani na Lushoto leo na kuwataka kufanya kazi kwa uwadilifu weledi na utumishi katika kuwatumika wananchi katika nafasi zao walizopewa za kumuwakilisha Rais Samia.

Hayo ameyasema wakati wa hafla ya kuwaapisha wakuu hao wa wilaya katika ukumbi wa Halimashauri ya Wilaya ya Handeni ambapo amesema kuwa anategemea ubunifu katika utekelezaji wa majukumu yao sambamba na kutatua kero za wananchi.

“Nategemea nyie wakuu wa wilaya mtakua chachu ya maendeleo katika kukuza uchumi wa vipato vya wananchi kwenye maeneo yenu kwa kuibua fursa mbalimbali za kiuchumi hususani kilimo na viwanda”amesema RC Batilda.

Hata hivyo Mkuu wa Wilaya ya Lushoto, Japhar kubecha amesema kuwa anakwenda kushirikiana na wananchi wa wilaya hiyo Kwa ajili ya kuwaletea maendeleo lakini na kusimamia utekelezaji wa miradi ya maendeleo iweze kuwa ni yenye ubora.

Nae Mkuu wa Wilaya ya Pangani, Mussa Kilakala amesema kuwa kutokana na Pangani kuwa kwenye ukanda wa Pwani anakwenda kutekeleza kwa vitendo sera ya uchumi wa bluu Ili iweze kuleta tija kwa wananchi sambamba na kuongeza mapato zaidi

South Africa's Former President Sends SHOCKWAVES - Big SECRETS Revealed

 Students and alumni interact with Dr. Thabo Mbeki, the Patron of the Thabo Mbeki Foundation and Chancellor of Unisa, discussing a wide range of socio-political matters concerning the country, the continent, and the globe.

Engaging in a conversation with the former President, Dr. Thabo Mbeki.

Wednesday, March 13, 2024

HEKO MAKONDA TUME IMEONGEA NA WANANCHI.

Leo tarehe 13/3/2024 hapa Sapiwi wilaya ya Bariadi tumepokea tume iliyoundwa na mkuu wa mkoa wa Simiyu kufuatia agizo la Mwenezi Paul Makonda Putin. Ikumbukwe kuwa kulikuwa na mgogoro wa ardhi kati ya wananchi na chuo Cha IFM kufuatia upanuzi wa chuo uliopelekea kutwaliwa kwa maeneo ya wananchi kwa fidia ndogo bila kufuata utaratibu. Wananchi walipeleka kilio chao kwa Makonda alipofika mkoani Simiyu na kusikiliza kero hiyo na kuona kweli wananchi wanapunjwa na kuamuru mkuu wa mkoa aunde tume. Leo tume imefika kijijini na kuongea na wananchi ili kusikiliza kero,wananchi wameongea kwa uwazi na tume imekuwa makini sana kusikiliza na kutembelea maeneo kujionea uhalisia. Tume imeahidi kutoa ripoti yenye haki,usawa na isiyomuumiza mwananchi mnyonge. Tunasubiri kupokea majibu ya furaha kwani mkuu wa wilaya alibeza wananchi hao akisema wamewekwa TEGESHA wakati chuo kimewakuta pale. HEKO MAKONDA kwa kujali wanyonge.Heko serikali sikivu ya mama Samia

UWEKEZAJI KWENYE SEKTA YA ELIMU LAZIMA UMGUSE MWALIMU – DKT. BITEKO

📌 Azindua programu ya Kuboresha Kada ya Ualimu nchini (GPETSP)


📌 Ataja ongezeko la ajira kwa Walimu, madaraja na Bajeti ya Elimu


📌 Aeleza vipaumbele 8 kuendeleza Kada ya Ualimu


📌 Ataka Walimu wawe na Siku Maalum ya Motisha


📌 JK atoa neno kuhusu Taasisi ya GPE


Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema kuwa, uwekezaji wowote unaofanywa katika Sekta ya Elimu lazima umguse Mwalimu kwani ndiye injini na kiongozi wa rasilimali zote zinazowekwa kwenye mfumo wa elimu nchini.


Dkt. Biteko mesema hayo tarehe 13 Machi 2024 wakati alipomwakilisha Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan katika hafla ya kuzindua Programu ya Kuboresha Kada ya Ualimu nchini (GPETSP) katika Ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam hafla ambayo ilienda pamoja na kaulimbiu ya Walimu Wetu Fahari yetu.

“Mwalimu ndiye rasilimali kuu inayofanya rasilimali nyingine ziweze kuleta matokeo chanya kwenye Sekta ya Elimu, ndio maana mtaona programu tunayoizindua leo inaonesha kwa vitendo kuwa Serikali tunatambua kwamba lazima tuwekeze zaidi kwa Walimu  kwenye mazingira ya kujifunza na ufundishaji lakini pia kuwatambua Walimu kuwa ninyi ndio watu tunaowategemea kufanya elimu yetu iweze kwenda mbele.” Amesema Dkt. Biteko

 

Amesema, Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan anafanya kila jitihada ili masuala yote yanayowahusu Walimu yafanyiwe kazi kwa kasi ikiwemo kuwapunguzia changamoto zinawazowakabili ili Walimu hao wajikite katika kusomesha na kutatua changamoto za watoto mashuleni.


Ameongeza kuwa,  kutokana na kazi nzuri ya Walimu hapa nchini, ufaulu wa wanafunzi kutoka Shule ya Msingi kwenda Sekondari umeongezeka kutoka 907,802  mwaka 2021 hadi 1,092,984  mwaka 2023 ikiwa ni ongezeko la asilimia 20.4.


Dkt. Biteko ameeleza kuwa, Serikali inaendelea kuboresha bajeti ya Elimu ambapo katika mwaka 2021 fedha iliyotolewa ni shilingi Trilioni 4.7 na  kwa mwaka 2023 imeongezeka hadi shilingi Trilioni 5.7 sawa na asilimia 20.4.


Kuhusu  ajira kwa Walimu amesema kuwa, zimeongezeka ambapo katika kipindi cha Serikali ya Awamu ya Sita  Walimu 37,473 wa Sekondari na Msingi wameajiriwa,  Walimu 227,383 wamepandishwa madaraja na Walimu 20 wamebadilishiwa vyeo.


Amesema pamoja mafanikio hayo bado kuna changamoto kwenye Sekta ya Elimu ikiwemo ya kuongezeka kwa udahili wa wanafunzi ambao unahitaji ongezeko la Walimu na miundombinu mingine ikiwemo madarasa na nyumba za Walimu na kueleza kuwa Serikali inatambua bado kuna kazi kubwa ya kufanya katika Sekta ya Elimu ambapo ametoa wito kwa wadau kushirikiana na Serikali ili kuimarisha mahitaji ya Elimu nchini.


Dkt. Biteko amesema kuwa, Serikali ya Awamu ya Sita inawajali Walimu nchini na ndio maana inatekeleza vipaumbele Nane ili kuboresha kada hiyo ikiwemo ujenzi wa nyumba za Walimu kwenye Halmashauri za pembezoni, kuimarisha mfumo wa motisha kwa walimu  ili kuwafanya wabaki kwenye kazi yao, kuwezesha uandaaji wa mfumo jumuishi wa kieletroniki wa uandaaji, usimamizi na upangaji wa Walimu kwa kuzingatia usawa wa kijinsia na kuwezesha utekelezaji wa mpango wa ajira kwa walimu wa kujitolea kwa ajili ya kupungiza changamoto za upatikanaji wa walimu msingi ili kuimarisha mazingira ya kujifunza na ufundishaji.


Ametaja vipaumbele vingine kuwa, ni kumwezesha Mwalimu kufanya upimaji wa kielektroniki ili kupata matokeo ya kila hatua ya kujifunza, kujenga vituo vya walimu na kuweka samani na vifaa vya kielektroniki ili kuwezesha mafunzo endelevu kwa walimu waliokazini, ununuzi wa zana na vifaa visaidizi kwa Wakufunzi, Walimu, Walimu tarajali na wanaofundisha wanafunzi wenye mahitaji maalumu pamoja na kutoa ufadhili wa masomo kwa walimu wanaofundisha wanafunzi wenye mahitaji maalum.


Dkt. Biteko amempongeza Mwenyekiti wa Bodi ya Taasisi ya Kimataifa inayoshughulikia Masuala ya Elimu Duniani (GPE), Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete na kueleza kuwa nafasi aliyonayo ni heshima kwa nchi pamoja na Sekta ya Elimu nchini kwani amekuwa na mchango katika kuhakikisha nchi inafaidika na mfumo wa GPE ambao unahudumia nchi 89 duniani.


Katika hatua nyingine, Dkt. Doto Biteko ameziagiza Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia pamoja na TAMISEMi kuangalia utaratibu mzuri wa kuwapa motisha Walimu na hii ikihusisha kutenga walau siku moja ya kuwapa Motisha walimu hao badala kusubiri Mei Mosi kwa lengo la  kupata matokeo yaliyo bora kwenye Sekta ya Elimu.  

Awali, Mwenyekiti wa Bodi ya Taasisi ya Kimataifa inayoshughulikia Masuala ya Elimu Duniani (GPE), Rais Mstaafu wa Serikali ya Awamu ya Nne, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete alisema kuwa, lengo la Taasisi hiyo ni kusaidia kuchochea maendeleo ya elimu  katika nchi zinazoendelea hasa za kipato cha chini na za kipato cha kati hatua ya kwanza ambapo Tanzania ni moja ya nchi 89 wanufaika wa GPE.


Amesema kuwa, kutoka GPE ianze mwaka 2002 imeshachangia Dola za Marekani milioni 330  nchini Tanzania na kwamba GPE inaunga mkono juhudi za Serikali kuboresha Sekta ya Elimu ili kila mtoto nchini awe na ujuzi na maarifa na sasa Taasisi hiyo imeidhinisha ufadhili wa Dola za Marekani Milioni 80 kwa ajili ya programu ya GPETSP.

Awali, Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Adolf Mkenda alisema kuwa, programu iliyozinduliwa ya GPETSP inagusa sehemu mbalimbali katika Kada ya Ualimu ikiwemo kuhakikisha kunakuwa na utoshelevu wa  Walimu, ubora, uwepo wa miundombinu, vitendea kazi, kuendeleza makazi ya walimu  na motisha kwa walimu na kwamba Serikali imekuwa ikiyafanyia masuala hayo lakini GPETSP inakuja kuongeza nguvu na  kasi ya utekelezaji wa programu za Serikali ikiwemo Sera ya Elimu.





MWANZA YAVUNJA REKODI MAADHIMISHO YA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI

 

NA ALBERT G.SENGO/MISUNGWI/MWANZA Kauli mbiu ya ‘Siku ya Kimataifa ya Wanawake Duniani’ mwaka huu inasema 'Wekeza kwa Wanawake kuharakisha maendeleo ya taifa na ustawi wa jamii', ikiwa ni utejelezaji wa Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDG’s-2030) likiwemo la usawa wa jinsia, kupunguza tofauti ya kiuchumi na kutokomeza umaskini.

KIOMONI BINGWA ODO UMMY CUP 2024

 

Waziri wa Michezo,Sanaa na Utamaduni Dkt Damas Ndumbaro kushoto akimkabidhi Kombe la Mashindano ya Odo Ummy Cup Nahodha wa timu ya Kiomoni FC mara baada ya  kuibuka Mabingwa kwa kuifunga Nguvumali FC penati 3-1 kwenye mchezo wa fainali uliochezwa kwenye uwanja wa CCM Mkwakwani mjini Tanga juzi ambapo mshindi huyo alipatiwa pia kitita cha Sh Milioni 3,pikipiki ya magurudumu matatu,Ng’ombe,Jezi Seti pamoja na mpira  kulia ni Mbunge wa Jimbo la Tanga (CCM) Ummy Mwalimu ambaye pia ni Waziri wa Afya ambaye ndie muandaaji wa Mashindano hayo kushoto ni Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Tanga Rajab Abdurhaman

Na Oscar Assenga, TANGA

TIMU ya Kiomoni FC wametawazwa kuwa Mabingwa wapya wa Michuano ya Kombe la Odo Ummy Cup baada ya kuibamiza timu ya Nguvumali FC penati 3-1 katika mchezo wa Fainali uliochezwa kwenye uwanja wa Lamore Jijini Tanga.


Kutokana na ushindi huo waliweza kujinyakulia kitita cha Sh.Milioni 3,Pikipiki yenye Magurudumu matatu,Ng’ombe,Jezi Seti pamoja na mipira huku Mshindi pili timu ya Nguvumali FC waliweza kujinyakulia kitita cha Sh. Milioni 2.5 na Mpira na Jezi Seti 1.


Michuano hiyo ya Odo Ummy Cup huchezwa kila mwaka kwa kushirikisha kata zote za Jimbo la Tanga yakiwa na lengo la kuibua vipaji na kukuza kiwango cha soka kwa vijana ambao kupitia mpira wanaweza kujikwamua kiuchumi.


Mchezo huo ambao ulikuwa wa aina yake ambapo kila timu iliingia uwanjani hapo ikitaka kuibuka na ushindi ili kuweza kuchukua ubingwa wa michuano hiyo ambapo mpaka timu zote zinakwenda mapumziko zilitoka sare tasa.


Kipindi cha pili kilianza kwa kasi ambapo kila timu iliingia ikiwa na hari kubwa kutokana na kufanya mabadiliko kwa baadhi ya wachezaji wake ili kuweza kujiimarisha kwa lengo la kufanya vizuri katika michuano hiyo.


Wakionekana kucheza kwa umahiri mkubwa Kimoni FC walianza kwa kulishambulia lango la wapinzani wao bila kuwepo kwa mafanikio yoyote ambapo kila wachezaji walipokuwa wakipiga mashuti langoni mwao liligonga mwamba na kutoka nje.


Kutokana na ushindani wa mchezo huo ulizilazimu timu zote kutoka uwanjani dakika 90 bila kuona milango ya kila mmoja na hivyo mwamuzi wa mchezo huo kulazimika kupelekea mchezo huo kwenye mikwaju ya penati ambao ndipo kiomoni waliposhinda mabao hayo.


 Akizungumza mara baada ya kumalizika kwa mcheo huo wa Fainali Waziri wa Michezo,Sanaa na Utamaduni aliwapongeza waandaaji wa mashindano hayo huku akieleza kwamba mashindano ikiwemo Mbunge Ummy Mwalimu.


“Ukiona vyaelea ujue vimeundwa hili ya leo tuna kila sababu ya kumshukuru na kumpongeza Mbunge wetu Ummy Mwalimu niseme kama Waziri mwenye thamana ya michezo nimeshahudhuia mashindano yanayoandaliwa na wabunge mwengi sana sijaona mashindano mazuri kama haya”Alisema


Alisema mashindano haya ni mazuri na makubwa ambayo sijapata kuyaona katika maeneo mengine na Mbunge Ummy ana sifa ya kipekee kwa kuwajali wananchi wa Jimbo lake kutokana na kuhakikisha anawapigania ili kuweza kuondoa kero zenu.


Aidha alisema wanaposema michezo ni ajira wanaamini pia ni uchumi na wao kama Wizara wamemua hivi sasa michezo ni ajira na uchumi hivyo mashindano kama hayo watashirikiana na waandaaji kuhakikisha wanaibua vipaji na kuviendeleza.


Hata hivyo alisema kwamba mkoa wa Tanga ndio chimbuka la vipaji na wao serikali wataendelea kuiangalia Tanga huku akieleza kwamba Mbunge Ummy amepeleka ombi kwao kwamba uwanja huo wa Lamore ambao umechezewa fainali hiyo upandwe nyasi uwe mzuri ili fainali za mwakani ziwe nzuri .


“Na mimi nimemuhaidi Mbunge Ummy kwamba nitawaleta wataalamu kufanya tathimini  ili uwanja uweze kuwa katikaa hali nzuri kutokana na kwamba umuhimu wa mashindano hayo ya Odo Ummy Cup”Alisema


Awali akizungumza katika fainali hiyo ,Mbunge wa Jimbo la Tanga (CCM) Ummy Mwalimu ambaye ni Waziri wa Afya alisema kwamba suala la Odo Ummy Cup ni mchango wake katika kutekeleza ilani ya CCM ibara ya 243 ambayo inawataka kuwekeza kwenye mpira wa migu hasa kwa vijana.


Alisema wanamshukuru pia Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Tanga Comred Rajab Abdurhaman kutokana na kwamba amekuwa akiwasaidia na kuwaleta na kuwaongoza kwenye kutekeleza ilani.


Aidha alisema mashindano hayo lengo ni kuwaleta pamoja vijana wa Tanga mjini na  yameleta moja,mshikamano na hamasa ya kumweka karibu na vijana huku akishukuru timu zote kutoka Kata 27 ambazo zilishiriki kwenye michuano hiyo.


“Lakini pia nishukuru kamati za Siasa za CCM kwa kujitoa kusimamia mashindano hayo pamoja na timu ya Hamasa ya UVCCM pia niwashukuru wadhamini wetu kwa kuuunga mkono wakiwemo wadau wetu Assemble Insurance kwa kutuunga mkono”Alisema 


Hata hivyo kwa upande wake,Mwenyeiti wa CCM Mkoa wa Tanga Comred Rajab Abdurhaman atumia fursa hiyo kuwataka wabunge na madiwani wa mkoa huo wahakikisha wanaendelea michezo katika maeneo yao.


“Kwani kufanya hivyo ni kutekeleza kwa vitendo ilani ya CCM ambayo tumehaidi kuendeleza michezo hivyo lililofanyika linatafsiri ilani kwa vitendo hivyo wabunge na madiwani hakikisheni hili linatekelezwa”Alisema

KATIBU WA CCM MKOA WA PWANI AWAHIMIZA WANANCHI MSANGANI KUMCHAGUA GUNZE


NA VICTOR MASANGU/KIBAHA


Katibu wa Chama cha mapinduzi (CCM) Mkoa wa Pwani Bernard  Elias Ghati amewahimiza wana ccm pamoja na wananchi kwa pamoja  kumchagua kwa kishindo  mgombea wa udiwani kata ya Msangani Gunze Yohana  ili aweze kuwaletea wananchi maendeleo.

Katibu huyo ameyasema hayo wakati wa mkutano wa kampeni wa hadhara kwa ajili ya kuweza kumnadi mgombea wa udiwani uliofanyika katika mtaa Garagaza.


Katika mkutano huo wa kampeni ambao ulihudhuliwa na viongozi mbali mbali wa ngazi ya Wilaya pamoja na ngazi ya Mkoa sambamba na wananchi wengine kutoka Jimbo la Kibaha mjini.
Katibu huyo aliwaomba katika kuelekea katika uchaguzi huo wananchama wa ccm wanapaswa kuwa kitu kimoja katika kuhakikisha kwamba wanashinda kwa kishindo kwa asilimia kubwa katika uchaguzi huo.

"Kikubwa tunakuja katika mikutano hii kwa ajili ya kuzungumza mambo mbali mbali ambayo chama cha mapinduzi mambo ambayo yamefanyika katika utekelezaji wa Ilani hivyo wananchi wa Msangani inabidi kumchagua mgombea wetu Gunze '"alisema katika huyo.

Aidha katibu huyo alisema kuwa wana ccm wanatakiwa kuungana kwa pamoja na wananchi wote wa kata ya Msangani kwa lengo la kuwaeleza mambo mbali mbali yaliyofanyika ya kimaendeleo.
"Inatakiwa wana msangani wote muelewe shughuli mbali mbali za kimaendeleo  ambazo zimefanywa na hivyo ninawaomba wananchi kumchagua Gunze awe diwani wa kata ya Msangani,"alisema Katibu huyo.


Katika hatua nyingine aliongeza kuwa endapo wananchi wa kata ya Msangani wakimchagua Gunze kuwa diwani wa Kata ya Msangani ataweza kuwaletea maendeleo wananchi katika nyanja mbali mbali ikiwemo maji,afya,elimu pamoja na maeneo mengine.

Uchaguzi wa kujaza nafasi ya udiwani katika kata ya Msangani amnayo ilikuwa wazi unatarajiwa kufanyika machi 20 mwaka huu.

Monday, March 11, 2024

MWANZO MWISHO SIMULIZI SABABU ZA KIFO HATIMAYE MAZISHI YA NASSIB MABROUK JIJINI MWANZA

 NA ALBERT G. SENGO/MWANZA

Mamia ya mashabiki wa soka na waombolezaji wamejitokeza kwa wingi hii leo nyumbani kwa marehemu Nassibu Mabrouk, Kiseke wilayani Ilemela mkoani Mwanza, kwaajili ya sala hatimaye mazishi nayo kufanyika katika makaburi ya Kiseke B, wilayani humo. Nassibu Mabrouk aliyewahi kuhudumu kwa mafanikio kama Katibu wa Chama cha soka mkoa wa Mwanza (MZFA) alifariki dunia ghafla siku ya ijumaa akiacha maswali mengi kwa waliomfahamu. Juma Msaka ni mwenyeki wa mtaa alioishi marehemu Nassib Mabrouk anasimulia aliyoyajua hadi umauti ulipo mkuta.

Sunday, March 10, 2024

STATUS ZAFICHUKA - MABROUK NI KAMA ALIKITABIRI KIFO CHAKE ASEMA KABAGO KATIBU WA SIMBA MWANZA

 NA ALBERT G. SENGO/MWANZA

Mamia ya mashabiki wa soka na waombolezaji wamejitokeza kwa wingi hii leo nyumbani kwa marehemu Nassibu Mabrouk, Kiseke wilayani Ilemela mkoani Mwanza, kwaajili ya sala hatimaye mazishi nayo kufanyika katika makaburi ya Kiseke B, wilayani humo. PHILBERT KABAGO NI KATIBU WA SIMBA MWANZA NAYE AMEPATA NAFASI KUZUNGUMZA NA MWANAHABARI WETU GSENGO WA JEMBE FM

MCHENGERWA ATEMA CHECHE UFUNGUZI RASMI WA KAMPENI KATA YA MSANGANI

 


NA VICTOR MASANGU, KIBAHA

Waziri wa nchi Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na serikali za mitaa (TAMISEMI) Mohamed Mchengerwa amewataka wana CCM kuhakikisha kwamba wanaungana na kuwa kitu kimoja kwa lengo la kuweza kuibuka na ushindi katika uchaguzi wa kuchaza nafasi mbali mbali za udiwani katika Mkoa wa Pwani ambazo zimeachwa wazi kutokana na sababu mbali mbali.

Mchengerwa ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Rufiji na mjumbe wa Halmashauri kuu ya chama cha mapinduzi (CCM) Taifa aliyasema hayo wakati wa ufunguzi rasmi wa kampeni ya udiwani katika kata ya Msangani iliyopo katika Halmashauri ya mji Kibaha.

Katika ufunguzi wa kampeni hizo ambazo ziliweza kuhudhuliwa na viongozi mbali mbali wa CCM  kutoka katika kata zote 14 za Jimbo la Kibaha mjini pamoja na viongozi wengine kutoka ngazi ya Wilaya pamoja na Mkoa wa Pwani ikiwa sambamba na wananchi ambao waliweza kufika kwa kwa lengo lengo la kwenda kusikiliza sera za chama.

Mchengerwa alisema kwamba kwa sasa katika kuelelea chaguzi hizo inapaswa kumpa ushirikiano wa kutosha mgombea wa udiwani ili pindi atakaposhinda aweze kushirikiana na viongozi wengine katika kuwaletea wananchi chachu ya maendeleo.

"Kwa kweli tuna kila sababu kwa wana ccm wote kufanya kazi kwa bidii kuhakikisha kwamba wagombea wote waliopitishwa na chama cha mapinduzi na kupendekezwa katika vikao halali kuwashika mkono na kufanya kazi nyumba hadi nyumba kwa lengo la kuweza kuweka misingi mizuri ya kushinda kwa kishindo,"alisema Mchengrwa.

Ameongeza kwamba katika Mkoa wa Pwani kuna kata tatu ambazo kwa sasa bado zipo wazi ikiwemo kata ya Msangani hivyo ameahidi kushirikiana na wanachama wenzake katika kuelekea uchaguzi huo ili kuweza kushinda na kuwahimiza wanachama wa ccm kuwa kitu kimoja hasa katika kipindi hiki.



Kadhalika alisema kwamba hakuna sababu za kupoteza nafasi hizo kwa kata ambazo zimeachwa wazi kwani Rais wa awamu ya sita Dkt. Samia Suluhu Hassan ameweza kuleta mafanikio na maendeleo makubwa kwa wananchi hivyo kuna kila sababu ya kushinda kwa kishindo katika uchaguzi huo.

"tunapozungumzia maendeleo maana yangu ni kwamba Rais Samia ameweza kufanya mambo makubwa kutokana na kupeleka fedha nyingi ambazo zimekwenda katika kutekeleza miradi mbali mbali ya maendeleo katika kata ya Msangani ikiwemi miradi ya elimu, afya, miundombinu ya barabara umeme na miradi mingn=ine,"alisema Mchengerwa.

Pia Mchengerwa alisema kwamba viongozi wa CCM pamoja na diwani wa kata ya Msangani ambaye atachaguliwa katika uchagauzi huo wanatakiwa kuwafikia wananchi kwa wakati kwa kuhakikisha kwamba  wanakwenda kusikiliza kero mbai mbali ambazo zinawakabili wananchi ili kuweza kuzitafutia ufumbuzi.

"ndugu zangu nimekuja hapa kata ya Msangani lakini kitu kikubwa nawataka viongozi wa ccm hsa wale wa kuchaguliwa kufanya kazi kwa bidii na kuhakikisha wanatetea maslahi ya wananchi wake na sio kwa ajili ya matumbo yao binafsi na hili jambo ni muhimu sana ndio maana nimewaambia,"alisema Mchengerwa.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa chama cha mapinduzi (CCM) Wilaya ya Kibaha mji mwalimu Mwajuma Nyamka  alisema  kwamba  viongozi  na wanachama wa ccm  wanatakiwa  kuvunja kabisa makundi yote na kuhakikisha wanakuwa kitu komoja kwa ajili ya kukiimarisha chama kuanizia ngazi za chini hadi za juu.

Naye mgombea wa nafasi ya udiwani katika kata ya Msangani Gunze Yohana amewahidi wananchi wa Msangani pindi atakoshinda katika uchaguzi huo kushirikiana nao bega kwa bega katika kuwasikiliza kero mbali mbali zinazowakabili ili aweze kuzifanyia kazi na kuzitatua.

Kadhalika aliongeza kuwa changamoto ambazo zinawakabili wananchi wa Msangani anazitambua vizuri hivyo ana imani kubwa endapo akiweza kuchaguliwa atazichukua kwa kuzishughulikia kwa haraka ikiwa pamoja na kuleta miradi mbali mbali ya maendeleo ambayo itaweza kugusa katika nyanja mbali mbali.

Uchaguzi wa kujaza nafasi ya udiwani katika kata ya Msangani katika halmashauri ya mji Kibaha pamoja na maeneo mengine yaliyokuwa wazi unatarajiwa kufanyika mwezi machi mwaka huu katika Wilaya tatu za Mkoa wa Pwani ambazo zilikuwa zimeachwa wazi kutokana na sababu mbali mbali.

Saturday, March 9, 2024

MABANGO NA UJUMBE MAADHIMISHO SIKU YA WANAWAKE DUNIANI MISUNGWI MKOANI MWANZA.

aaaa
Mamlaka ya Usimamizi wa wanyamapori Tanzania TAWA - Wekeza kwa wanawake Kuharakisha Maendeleo ya Taifa na Ustawi wa Jamii

Shirika la Umeme Tanzania - Wekeza kwa wanawake Kuharakisha Maendeleo ya Taifa na Ustawi wa Jamii
Wizara ya \Uchukuzi na Huduma za Meli - Wekeza kwa wanawake Kuharakisha Maendeleo ya Taifa na Ustawi wa Jamii
Wadau Halmashauri ya Misungwi - Wekeza kwa wanawake Kuharakisha Maendeleo ya Taifa na Ustawi wa Jamii
Idara ya Uhamiaji Mwanza - Wekeza kwa wanawake Kuharakisha Maendeleo ya Taifa na Ustawi wa Jamii
TAHEA MWANZA - Wekeza kwa wanawake Kuharakisha Maendeleo ya Taifa na Ustawi wa Jamii.
Wizara ya utamaduni, sanaa na Michezo - Wekeza kwa wanawake Kuharakisha Maendeleo ya Taifa na Ustawi wa Jamii
Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu NIMR - Wekeza kwa wanawake Kuharakisha Maendeleo ya Taifa na Ustawi wa Jamii
Mahakama ya Tanzania Kanda ya Mwanza - Wekeza kwa wanawake Kuharakisha Maendeleo ya Taifa na Ustawi wa Jamii.
Mamlaka ya maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali - Wekeza kwa wanawake Kuharakisha Maendeleo ya Taifa na Ustawi wa Jamii

 Wekeza kwa wanawake Kuharakisha Maendeleo ya Taifa na Ustawi wa Jamii

WANAWAKE SF GROUP WAMWAGA MISAADA SHULE YA SEKONDARI KOKA, WATOTO YATIMA NA HOSPITALI YA LULANZI

 
VICTOR MASANGU,KIBAHA 

WANAWAKE wa kampuni ya SF group ya Jijini Dar es Salaam wameadhimisha kilele  cha siku ya mwanamke duniani kwa kufanya matendo ya huruma kwa kutoa msaada katika maeneo mbali mbali ya Jimbo la Kibaha mjini.

Wanawake hao wa SF group  wameweza kutembelea katika nyanja mbali mbali ikiwemo sekta ya elimu,afya pamoja ya mambo kuwatembelea watoto wenye mahitaji maalumu.

Katika maadhimisho hayo wanawake wa SF Group ambayo ndani yake kuna makampuni mbali mbali ambayo  yamekuwa mstari wa mbele katika kusaidiana na jamii.
Mkurugenzi wa Rasirimali watu wa SF Group Maria Faustine ambaye aliongoza jopo la wanawake hao walikwenda kutoa msaada wa vifaa mbali mbali  katika shule ya sekondari Koka.

Mkurugenzi huyo alibainisha kwamba wameamua kwenda kutoa vifaa katika shule hiyo ya Koka ikiwa ni katika kuwasaidia wanafunzi7 kupata mahitaji yao hususan kwa upande wa  wanawake.

"Tumeungana wanawake wote wa SF Group katika kuadhimisha kilele cha siku ya wanawake duniani kwa kutembelea maeneo matatu  ikiwemo shule ya Koka,watoto yatima pamoja na hospitali ya Lulanzi,"alisema Mkurugenzi Goleti.

Kadhalika aliongeza kuwa katika kuunga mkono juhudi  za serikali awamu ya sita katika kuboresha sekta ya elimu wameamua kutoa zawadi kwa msichana mwanafunzi aliyefanya vizuri katika masomo yake.
Pamoja na hayo walikwenda kutembelea kituo cha watoto yatima cha Buloma kilichopo kata ya Picha ya ndege na kutoa msaada wa mahitaji mbali mbali ya msingi ikiwemo vyakula mbali mbali kama sukari,unga pamoja na  sabuni,madaftari na mambo mengine ya msingi.

Kadhalika sambamba na hayo waliweza kutembelea katika Hospitali ya Wilaya ya Lulanzi ambapo pia waliweza kutoa msaada wa vitu mbali mbali  kwenye wodi ya wazazi.

Mkurugenzi Faustine alibainisha kuwa lengo kubwa la kwenda kutoa msaada katika maeneo matatu ni kwa ajili kuonyesha ushirikiano wa dhati kati ya wanawake wa SF Group pamoja na jamii.
Kwa upande wake mwalimu mkuu wa shule ya Koka Sekondari Magreth William aliwashukuru kwa dhati wanawake hao wa SF Group kwa msaada huo pamoja na Mbunge wa Jimbo hilo Silvestry Koka kwa sapoti katika mambo mbali mbali.

Kadhalika nao  baadhi ya watoto wanaoishi katika mazingira magumu katika kituo hicho cha Buloma walitoa shukrani zao za dhati kwa msaada huo kutoka kwa wanawake wa SF Group.
Nao badhi ya viongozi wa chama cha mapinduzi (CCM) ambao walishiriki katika zoezi  hilo la ugawaji  hawakusita kutoa shukrani zao za dhati kwa wanawake  hao wa SF group.


SF Group imetumia kilele cha maadhimisho ya siku ya mwanamke duniani kufanya matendo ya Huruma katika sehemu tatu.shule ya Sekondari Koka.kituo cha watoto yatima Buloma na wodi ya wazazi katika Hospitali ya Wilaya Lulanzi.